Wednesday, February 5, 2020

MWANADAMU PASIPO MUNGU SI CHOCHOTE


MWANADAMU PASIPO MUNGU NI SAWA NA KAZI BURE















FLAVIAN J. LUTAKANGWA




YALIYOMO




DIBAJI

SHUKRANI

UTANGULIZI

“Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutani! Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake? Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena? Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.”[1]  
Isa 40:13 “ni nani aliyemwogoza roho ya Bwana, na kumfundisha kwa kuwa mshauri wake?” na Ayu 41:11 (Ni nani aliyetangulia kunipa hata nimlipe? Kila kilicho chini ya mbingu  nzima ni changu)



SURA YA KWANZA

UKO HURU?

Dakika ile ile ambapo Mungu humpatia mwanadamu uzima, humjalia pia uhuru wa kuchagua kati ya mema na mabaya. Uchaguzi wa mema ni matumizi mema ya uhuru, na uchaguzi wa mabaya ni matumizi mabaya ya uhuru. Mungu aliyetuweka katika njia panda yenye  barabara mbili ambazo yatubidi kuchagua kufuata mojawapo, alituamuru kutenda mema peke yake na ametukataza kinaganaga kutenda mabaya. Ni mahali gani tunakuta matakwa ya Mungu yanapotualika kutenda mema na ktukataza kabisa kutenda maovu? Katika Amri Kumi ambazo ni sheria za Mungu zilizoandikwa katika moyo wa kila mwanadamu. Kwa hiyo mtu anayezitii Amri za Mungu hutumia vema uhuru wake, na mtu asiyeshika Amri za Mungu hutumia vibaya uhuru wake.  Ni kwa manufaaa ya kila mtu kwamba azitii Amri za Mungu na kutumia vema kipaji hicho kikubwa cha uhuru aliojaliwa. Mungu aliahidi tuzo  kwa wau wema na aliahidi pia adhabu kwa watu watendao mabaya. Ili kwamba matumizi ya uhuru yawe mazuri, lazima tendo lenyewe liwe jema katika nadhumuni yaani katika nia njema na liwe limetendwa kwa wema na kwa namna ipatanayo na maadili mema. Yafaa kuongeza kusema kwamba matumizi mazuri ya uhuru ni fadhila, bali matumizi mabaya ya uhuru ni udhalimu. [2]
  Moyoni mwake mtu anatambua sheria isiyotoka kwake mwenyewe, ni sauti ya dhamiri inayomwamuru kufanya mema na kuacha mabaya. Dhamiri ni sheria ya iliyochapwa na Mungu mwenyewe moyoni mwa mtu. Kushika sheria hii ni kulinda cheo chake, kwani  mtu atahukumiwa kadiri alivyofuata sheria ya dhamiri yake. Kadiri dhamiri inavyokuwa na nguvu zaidi za kumwongoza mtu, kadiri hiyo hiyo atakuwa mwema zaidi. Pengine dhamiri inadanganyika ikitaja njia isiyo ya kweli, lakini ikiwa si kosa la mtu mwenyewe, cheo chake hudumu kwani ameshika amri ya Mungu iliyosema: fuata dhamiri yako.[3]
Kwa hiari tu mtu anaweza kuchagua wema. Uhuru kumbe ni jambo kubwa sana. Hasa siku hizi watu wanadai uhuru wao; ni haki yao, lakini mara kwa mara watu wanaangalia uhuru kama ruhusa ya kufanya kama wanavyotaka wenyewe mema au mabaya. Hii si maana ya uhuru; uhuru wa kweli ni alama kwamba mtu ameumbwa kwa mfano wa Mungu, ni alama kama Mungu ametaka mtu achague kwa hiari yake kati ya mema na mabaya, amchague Mungu na kwa uaminifu huo atapata heri.[4]  
“Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.”[5]
YBS 31: 25-31 JUU YA POMBE
Mungu alimwumba mtu kwa sura yake na akamfanya rafiki yake. Kama kiumbe cha kiroho, mtu hawezi kuuishi urafiki hu bila kujinyenyekea kwa hiari mbele ya Mungu. Hiyo ndiyo maana ya amri aliyopewa mtu asile matunda ya Mti wa Ujuzi wa Mema na Mabaya: “kwa maana siku utakapokula, hakika utakufa.”[6] Mti wa ujuzi wa mema na mabaya huonyesha kwa mifano mipaka ambayo mtu, kwa vile ni kiumbe, amewekewa asiivuke. Tena aikubali mipaka hiyo kwa hiari na aiheshimu kwa ujasiri. Mtu anamtegemea Muumbaji wake, na yuko chini ya sheria za uumbaji na taratibu za maadili zinazoratibu matumizi ya uhuru.[7]
Mtu akishawishiwa na ibilisi, aliliachilia tumaini alilokuwa nalo kwa Muumba wake life moyoni mwake, na kwa kutumia vibaya uhuru wake akakaidi amri ya Mungu. Hiyo ndiyo dhambi ya kwanza ya mtu. Tangu hapo, kila dhambi itakuwa ni kumkaidi Mungu na kukosa kutumainia wema wake.[8]
JISIMAMIE
“Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa Yule mwovu.”[9]
ISIKILIZE DHAMIRI
Hata haki za binadamu (The Universal Declaration of Human Rights art. 18), inadai kuwa mwanadamu ana haki ya uhuru wa kusikiliza dhamiri yake. DH 3, 7.

SURA YA PILI

ALIYEKUUMBA PASIPO WEWE HAWEZI KUKUOKOA PASIPO WEWE


Una kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa zawadi hii ya imani uliyonayo. Maana imani ni zawadi itokayo kwa Mungu mwnyewe. “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nfsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu” Efe 2:8-9
Kuzitanaza kazi za Bwana ni kumsifu Mungu, alisema Cassiodorus
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu. 1 Pet 2:9

Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru; kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; mkihakiki ni nini impendezayo Bwana. Efe 5:8-10.
Wajibu wako kama Mkristo.
Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu,bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwepo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopana kutetemeka. Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema. Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,, mpae kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,, mkishika neno la uzima; nipate sababu ya kuona fahari katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio bure wala sikujitaabisha bure. Naam, nikiminwa juu ya dhahabu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote. Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami. Flp 2:12-18

Juu ya uvumilivu
Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno. Yak 1:2-4. Tunaaswa katika majaribu tupatayo na imani yetu ikiwa imestahilika basi itatujalia uvumilivu. Na uvumilivu huu ndiyo utakawo tutegemeza mpaka mwisho wao hatutopungukiwa na chochote. Maana Mungu anatueleza kuwa kamwe hawezi kumjaribu mtu kupita uwezo wake. Tazama Ayubu alivyojaribiwa, lakini kwa imani aliyokuwa nayo akawa mvumilivu na mwisho hakupoteza chochote.
Kwahiyo, “Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.”         Efe 2:10


SURA YA TATU

MUNGU HAMTUPI MJA WAKE AU MTU AMTAFUTAYE


Ni kweli na ni wazi kuwa, mwanadamu yu katika kutafuta yaliyo mema na yenye kupendeza na kufurahisha. Maumivu, machungu na huzuni, si hali za kawaida na zilizozoeleka sana kwa mwanadamu japo hayo yote ni sehemu ya maisha yetu. Ndiyo maana hata Yesu alipaza sauti akilia pale msabani ilipopata saa tisa akisema “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” yaani “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”(Rej. Mt 27:46; Zab 22:1)  Mahangaiko yote aliyonayo mwanadamu, ni katika kutafuta furaha na Amani, japo yote hayo ni ya muda tu kama tunavyoambiwa na Mt. Augustino kuwa furaha ya kweli tutaipata pale tutakapokutana na Mungu. Kwa kila afanyacho mwanadamu, kwa kuzingatia lengo lake (purpose/end) ni chema kwa mhusika; japo ukiangalia kwa jicho la kimaadili unaweza kukuta ni kitu kibaya na ambacho pengine hakikutazamiwa kufanywa na mhusika. Lengo la kila anachofanya mwanadamu ni kupata furaha yeye, kasha na wote anaohitaji washirikine furaha hiyo.
Shida inakuja pale yanapotokea matokea hasi ya kile ambacho kwa kiasi kikubwa ni tofauti na kile kilicho tazamiwa. Ukweli ambao uko wazi kabisa kwa kila mtu, ni kwamba, katika kutafuta, kuna kupata na kukosa, katika kuomba kuna kupewa na kutopewa, hali kadhalika katika kugonga (kubisha hodi) kuna kufunguliwa ama lah! Pamoja na ukweli huu kuwa wazi,bado si rahisi kwa yeyote kupokea matokeo hasi ya alichokifanya. Sijui kwa asilimia zote,shida ni kwa hali hiyo kuwapo pale tukutanapo na matokeo hasi. Pengine ni fikiriacho ni kwamba; wanadamu tumejiwekea kizingiti cha ubinadamu ambacho hakitufanyi kuyafikiria yote yatupatayo katika jicho la kiroho pia. Nafasi ya Mungu imekuwa ni ndogo zaidi ya ubinadamu ambao tunaupa nafasi kubwa na kusahau kuwa hata Mungu aliyetujua hata kabla ya kuzaliwa kwetu anampango nasi “Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua…”[10]
Katika hali isiyo ya kawaida ya kuhisi uchungu na kuhuzunika kwa matokeo hasi ndiyo watu wanapojiona kuwa hawafai, hawana thamani mbele ya mtu Fulani na hiyo hupelekea watu wengi kujiuliza swali maarufu sana kuwa kikishakushinda, wakisema “kwanini mimi?” Wengi hujiuliza hivyo pale wanaposhindwa kutimiza malengo yao. Baada ya tafakari ya muda mrefu juu ya matumizi ya msemo huo, sijafanikiwa kupata jibu kamili. Hiyo ni kwa sababu naona, namna msemo huo unavyotumika si sahihi kabisa, kwa kuwa wengi huutumia kwa upande mmoja tu.Sijawahi kusikia, mtu yeyote aliyefanikiwa jambo Fulani hata kama ni mara kwa mara huwa anafanikiwa au pengine ni mara hiyo tu, akijiuliza, kwanini mimi? Katika maana kwamba, kwanini yeye afaulu, afanikiwe, ashinde na si wengine, ila wengi hujiuliza, kwanini mimi ndiyo nafeli, nashindwa, sifanikiwi, sipewi au sipendwi?
Kushinda ni sehemu ya maisha, na kushindwa halikadhalika ni sehemu ya maisha, yatupasa kila mmoja wetu kutambua kuwa, katika hayo yote kuna kitu yatupasa kujifunza. Yatupasa kwenda mbali zaidi pia nakuona kuwa, pale sisi tunapopanga kuhusu baadae, Mungu wetu alishapanga yake, na yatupasa kuwa tayari kuona yake yakitimia kwanza kabla yetu “Baba yangu, ikiwa haiwezezakani kikombe hiki kiniepuke nisipokunywa, mapenzi yako yatizwe”[11] Hamna haja ya kujilaumu na kujiona hufai, wewe ni wathamani hivyo ulivyo. Tusihangaikie ya mwili ili hali hatujui kuhusu roho zetu, “kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake?”[12] Je, kwa kuwa na malalamiko ya mara kwa mara, ni ishara ya wazi kwamba tunahisi kuwa Mungu hayuko tena upande wetu? Mbona Ayubu pamoja na fahari zake zote, ila yote yalitoweka na alikubal ihali halisi jambo lililompelekea kuishi kwa furaha hata katika hali yake hiyo ya pili aliyokuwanayo, “je, tupate mema mkononi mwa Mungu, na si tusipate na mabaya?” (Ayu. 2:10).
Ndugu zangu katika Kristo, maisha ni safari, na njia tuipitiayo kama tulihisi haina makorongo, kona, na milima, basi tulijidanganya, na sasa yatupasa kutambua kwamba, vilima, makorongo na kona, yote hayo yapo katika njia tuipitiayo. Pia lengo ya hayo si kutukatisha tamaa, bali ni kutuongezea umakini katika safari yetu. Tukiwa wakujilaumu mara zote, hakika tuna mhakikishia shetani kuwa ananguvu juu yetu, kwani lengo lake ni kutukatisha tamaa. Ili kukomaza  imani zetu  kwa Mungu, hatunabudi kupata majaribu na mateso kama ilivyokuwa kwaYesu katika kukamilisha mpango wa Baba wa ukombozi. Hata dhahabu hujaribiwa kwa moto ili kuipata dhahabu iliyo nzuri, je, si zaidi na si  katika kukomaza imani zetu? Kama wakristo, yatupasa kuchukulia mateso  na  majaribu katika mtazamo chanya, kwani hata kama kushindwa kwetu katika yale tunayoyapenda  yatutaletea kifo, kwetu  iwe ni  faida lakini yatokee katika hali itakayotupelekea kumpata Kristo. Mt. Paulo anasema, “kwa maana, kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.”[13] Tudumu katika imani, tudumu katika kumtegemea Mungu, na maisha yetu ya kila  siku yawe sehemu ya kujifunza nasi tumpe Mungu nafasi zaidi ya kututumia kadiri atakavyo. Katika yote tumkimbilie Mungu maana anatupa matumaini kuwa “Mkiniomba neno lolote kwa jina langu, nitalifanya”[14]
KWANINI TUJILAUMU
“Hawataona njaa, wala hawataona kiu; hari haitawapiga, wala jua, kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza. Nami nitafanya milima yangu yote kuwa njia, na njia kuu zangu zitatukuzwa zote. Tazama, hawa watakuja kutoka mbali, na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya Sinimu. Imbeni, enyi mbingu, ufurahi, ee nchi, pazeni sauti ya kuimba enyi milima, kwa kuwa Bwana amewafariji watu wake, naye atawahurumia watu wake walioteswa. Bali Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.” Je, mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.” [15]




SURA YA NNE

MWITO WA MUNGU KWA KILA MTU



SURA YA TANO

TUTUMIE MBINU NA NJIA ZA KISASA KUTATUA CHANGAMOTO ZA LEO NA WALA SIYO ZA KESHO

 Mt. Agustino wa Hipo Afrika ya kaskazini alisema, ishi leo kama vile kesho hutaiona



HITIMISHO

Mimi na wewe ni akina nani sasa? Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe,  wala kweli haimo mwetu.[16] Nasi hatuwezi kusema ya kuwa tuna maisha pengine bora au mazuri kwa jitihada na nguvu zetu. Maana anayetujalia nguvu zenyewe za kutenda hayo ndiye Mwenyezi Mungu. Kumbe yote tutendayo yampendezayo na kukubalika machoni pa Mungu ndiyo haki yake Mungu kwetu sisi wanadamu. “Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu. Kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia. Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani.  



REJEA



[1] Rum 11: 33-36
[2] Natale Defendini, Uhulisho na Ukombozi, Mawaidha kuhusu itikadi ya Kikristu, Mfasiri Samuel Loishiye Mollel, Chapa Ferrari, Italy, 1997, Uk. 218.
[3] Mtaguso Mkuu, Maelezo ya Hati 16 za Vatican II, “Hati juu ya Kanisa na Ulimwengu” Na. 16.
[4] Mtaguso Mkuu, Maelezo ya Hati 16 za Vatican II, “Hati juu ya Kanisa na Ulimwengu” Na. 17.
[5] Gal 5:13-14.
[6] Mwa 2:17.
[7] KKK Na. 396.
[8] KKK. Na. 397.
[9] Mt 5: 37.

[10] Rej. Yer. 1:5
[11] Rej. Mt. 26:42
[12] Mt. 16:26
[13] Flp 1:21
[14] Yn 14:14
[15] Isa 49:10-15.
[16] 1Yn 1:8.

UKRISTO WAKO UKO WAPI


UKRISTO WAKO UKO WAPI???














FLAVIAN J. LUTAKANGWA


 












VIFUPISHO

Eze                  Ezekieli
Flp                  Wafilipi
Hes                 Hesabu
Hos                 Hosea
Ibid                 Sawa na kilicho juu
Isa                   Isaya
KKK                Katekesimu ya Kanisa Katoliki
Kum                Kumbukumbu la Torati
Kut                  Kutoka
Law                 Mambo ya Walawi
Kol                   Wakolosai
Lk                    Luka
Mal                  Malaki
Mwa                Mwanzo                                                   
Mit                   Mithali
Mik                  Mika
MSK.               Mkusanyiko wa Sheria za Kanisa
Mt                    Mathayo
Mt.                   Mtakatifu
Na.                   Namba
n.k.                   Na kadhalika
Rej.                  Rejea
Rum                 Warumi
1 Sam              1 Samweli
1 Tim               1 Timotheo
Uk                    Ukurusa
Yer                   Yeremia
Yos                   Yoshua
1 Yoh               1 Yohane
2 Yoh               2 Yohane
Ybs                  Hekima ya Yoshua Bin Sira
Yn                    Yohane
Zab                   Zaburi
§                       Ibara
&                      Na
/                        Au

DIBAJI

SHUKRANI

UTANGULIZI

Mkristo maana yake ni mfuasi wa Yesu Kristo. Kumbe wale walio wafuasi wa Kristo ndiyo hao wanaitwa Wakristo. Mtu anaitwa Mkristo mara baada ya kupokea Sakramenti ya Ubatizo.[1] Ubatizo ni nini? Ubatizo haupingani na imani bali huandamana nayo (Gal 3:26-27; Efe 4:5; Ebr 10:22). Ubatizo ni alama wazi na nguvu ya mambo yanayotendeka ndani ya mtu. Paulo anahesabu imani na ubatizo kuwa na mapato yaleyale (Gal 2:16-20; Rum 6:3-9). Watu wa zamani hubatizwa kwa kutoswa majini, na maana ya neno la ubatizo kwa kiyunani ni kutosa majini. Tendo hili la kutoswa na kutoka majini latumika na Paulo kama mfano: kutoswa majini maana yake mkosefu azikwa pamoja na Kristo (Kol 2:12), kutoka majini maana yake mkosefu afufuka pamoja na Kristo (Kol 8:11) ili awe kiumbe kipya (2Kor 5:7) au mtu mpya (Efe 2:15), au viungo vya mwili mmoja vihuishwavyo na Roho mmmoja (1Kor 12:13). Ufufuko huo utakuja kukamilika mwisho wa dunia (1Ko 15:12).
Hivyo kulingana na Sheria za Kanisa la Kirumi, Mkristo anaanza kubanwa na sheria yule tu mwenye uelewa wa kutosha na mwenye kuanzia umri wa miaka saba.[2] Baada ya Ubatizo mwaliko kwetu sote ni kulitangaza Neno la Mungu kwa watu wote.[3]
Kwa hiyo, lengo la mwandishi wa kitabu hiki anataka kutuonyesha maisha yampasayo kuishi kama muumini Mkristo tena Mkatoliki. Ni kutokana na nia hiyo, mwandishi anakuwa na mtazamo juu ya kuwa na imani nawe msomaji wa kitabu hiki; kuwa kile utakachotoka nacho kama fundisho basi ukakigawe na kwa wengine. Kama Askofu Mkuu Furton Sheen alivyoongezea katika swali mahususi la kwanini Mungu alituumba. Yeye alisema ya kuwa Mungu ametuumba ili tumjue, tumpende, tumtumikie na kabla ya kwenda kwake mbinguni basi tugawiane na kupeana yale tuliyojifunza (tuwafundishe na watu wengine, na siyo kubaki nayo sisi wenyewe; huo utakuwa uchoyo na tutaonyesha wazi kwamba wengine hatutaki waweze kufika kwa Baba muumba wetu).
Mpangilio wa Kitabu
Kitabu hiki kina jumla ya sehemu nane. Sehemu ya kwanza inahusu Maneno. Sehemu ya pili inahusu utumishi kwa wote. Sehemu ya tatu inaongelea juu ya Matendo Sehemu ya nne inahusu Imani. Sehemu ya tano inazungumzia juu ya Sakramenti. Sehemu ya sita inahusu ukipenda dunia zaidi, kumpenda Mungu hakuko ndani yako. Na sehemu ya saba inaongelea juu ya Mpinga Kristo. Na sehemu ya mwisho inahusu juu ya wapi tumaini lako lilipo? Na mwisho mwishoni ni juu ya Hitimisho na Rejea.



SEHEMU YA KWANZA

MANANO TU

1.0 UTANGULIZI

Kuna methali isemayo “Mkono mtupu haulambwi” ukisema uishi kwa kufuata maneno tu ya watu, kwa hakika utapotoshwa. Unachopaswa kuangalia na kujiuliza ni je! maneno hayo yanatoka moyoni au mdomoni tu? Ukishatambua basi unakuwa katika hali iliyo njema. Na kitu cha pekee kitakachokufanya uone ya kuwa mtu huyu anachoniambia kitakuwa kina ukweli au kinatoka moyoni ni pale tu mhusika atakapo jieleza akiwa huru au akiwa amejiachia. Lakini tambua kuwa ni vigumu sana mtu afikie hatua hiyo, maana mwanadamu mara zote anakuwa ni mtu wa hofu sana. Inaweza ikawa hofu ya mamlaka, hofu ya uthubutu au hofu ya kitu chochote kile ambacho kwayo anafikiria juu ya matokeo yake itakuwaje.
Maneno huonyesha mtu, “kutikisa chekecheke, itabaki wishwa; vilevile ila za mtu katika kujadili. Tanuu hujaribu vyombo vya mfinyanzi; vilevile jaribio la mtu ni kujadili. Matunda ya mti huonyesha ulimaji wake; vilevile kujadili mawazo ya moyoni. Usimsifu mtu usijemsikia anajadili; hakika hilo ni jaribio la wanadamu.”[4] Aya hizi zinatuonyesha wazi kuwa ukitaka kumjua mtu na kwa namna ya pekee kupitia nafasi, embu jaribu umpe nafasi ya kuongea au kujadili naye. Kupitia maongezi au kujadili nae utagundua kile akisemacho kinatoka moyoni au mdomoni. Pia wakati wa majadiliano hayo jitahidi umpe uhuru, hiyo ndiyo nafasi pekee itakayompatia mwanya wa kufunguka kweli kweli.
Mfano huu wa kumpatia mtu uhuru ili aweze kuongea pasipo wasiwasi na bila kujibakiza, naufananisha na mfano wa mtoto mdogo. Mtoto mdogo anaweza akawa ametenda kosa fulani. Na kwa sababu mtoto mara zote ukimbananisha vizuri basi huwa anasema ukweli. Sasa ikatokea mtoto huyu kakosea au kuna kitu nyumbani hakiko sawa na pengine mtoto huyu alishiriki moja kwa moja au alishuhudia. Utakapo muuliza akwambie ilikuwaje na ukamhakikishia kuwa hutomfanya kitu chochote hata kama ni yeye aliyeharibu kitu hicho, basi atakwambia chanzo cha mkasa na namna ilivyotukioa mpaka mwisho. Kwa nini anafanya hivyo? Anaongea yote kwa kuwa umeshamtengenezea mazingira ya yeye kusema kile kilichotendeka kwa uwazi kabisa na ndicho hicho kitokacho moyoni.
Katika fundisho hilo hilo, tuchukulie mfano wa mtu mzima. Mtu mzima anatambua kilicho chema na kibaya pia. Kumbe anaweza akawa hajapendezwa na kitu fulani na akaogopa kumfuata mhusika, na badala yake kama ni mtu wa kutumia kamvinyo au kilevi basi anapotumia ni hali ya kawaida kuwa  anarudi katika asili. Yaani anakuwa huru na anatenda kama mtoto mdogo. Hivyo anaweza kuanza kuwaeleza rafiki zake alionao pale juu ya mtu Yule ambaye pengine anamkwaza katika maisha. Na hapo kile atakacho kuwa anakitoa kwa hakika chatoka moyoni. Au mwingine anachukizwa na mtu, ila hana au hawezi kumfuata na kumweleza. Badala yake anasema na kupanga pia kunuwia kwenda kumnywea pombe. Akijisemea leo atanitambua, na kweli anapokunywa na kukutana naye anamweleza kila kitu kutoka moyoni kabisa; maana anakuwa amerudi katika asili yake na hivyo kutomwonea aibu kwa kuwa anakuwa yuko huru. Ndiyo maana muda mwingine watu wanasema pombe inatabia ya kukata mshipa wa aibu. Ina maana sawa na mfano huo, kwa kuwa akishalewa basi hawezi kutunza siri na akianza kuongea karibu kila kitu anachokichukia au kukipenda katika maisha ataweza kukwambia.  
Kwa hiyo, tunatahadhalishwa sana kuwa na umakini katika maneno yetu. Lakini pia tuwe watu wa kuchuja maneno yetu kabla ya kusema. “Usijadiliane na mtu mwenye maneno mengi, ukaomekeza kuni juu ya moto wake.”[5] “Usipepete kwa kila upepo, wala usiipitie kila njia. Uwe mtu thabiti wa akili, na liwe moja neno lako. Uwe mwepesi wa kusikia, na mzito wa kutoa jibu.”[6]

1.1 Uthibitisho kupitia heri nane mlimani

“Heri walio maskini wa roho, maana ufalme wa mbinguni ni wao. Heri wenye huzuni, maana hao watafarijika. Heri wenye upole, maana hao watairithi nchi. Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watashibishwa. Heri wenye rehema, maana hao watapata rehema. Heri wenye moyo safi, maana hao watamwona Mungu. Heri wapatanishi, maana hao wataitwa wana wa Mungu. Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki, maana ufalme wa mbinguni ni wao.”[7]  Katika fikara za Yesu hao maskini ni watu wanyenyekevu kadiri ya (Sef 2:3). Maneno “wa roho” yanakosekana katika (Lk 6:20). Lakini hao maskini ni watu wasio na mali nyingi na watu wa kuonewa. Hali hiyoo yao huwaweka tayari kupokea ufalme wa mbinguni kwa urahisi bila pingamizi kubwa. Na hilo ndilo neno kuu katika hotuba hii juu ya heri (Lk 4:18; 7:22; Mt 11:5; Lk 14:13; Yak 2:5). Hali hii ya unyenyekevu ni sawa na utoto wa kiroho ambayo yahitajika sana katika kuingia ufalme wa mbingu (Mk 9:33 nk; Lk 9:46; Mt 19:13 nk). Ufalme wa mbingu ni siri waliyofumbuliwa wadogo (Lk 12: 32; 1Kor 1: 26 n.k). Maskini ni sawa na watu wanyonge watajwao katika Lk 1:48, 52; 14:11; 18:14; ni watu wa “mwisho” duniani hapa watakaokuwa watu wa “kwanza” katika ufalme wa mbingu (Mk 9:33); ni watu wadogo kwa kweli walio watu wakubwa (Lk 9:48; Mt 19:30; 20:26).
Ni kweli kwamba Kristo awadai tajiri na fukara umaskini wa roho. Lakini amesifu mara nyingi umaskini katika matendo. Na hasa huwadai wanafunzi ufukara katika matendo na si katika nia (maneno) tu (Mdo 2: 44; 4: 32; Mt 6: 9; 10: 9-10).  Yeye mwenyewe amekwisha tuonyesha mfano wa kuishi kifukara si kwa maneno bali matendo (Lk 2: 7; Mdo 8: 20) na kiunyenyekevu (Mt 11:29; Yn 13: 12 nk; Flp 2:7). Na akajifanya sawa na wadogo na watu duni (Mt 25: 45; 18:5).

SEHEMU YA PILI

UTUMISHI

2.0 UTANGULIZI

Yesu kuhani mkuu. “Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae; bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka. Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee. Maana ilitupasa sisi tuwe na kuhani mkuu wa namna hii: aliye mtakatifu, asiyekuwa na uovu, asiyekuwa na waa lolote, aliyetengwa na wakosaji, aliyekuwa juu kuliko mbingu; ambaye hana haja kila siku, mfano wa wale makuhani wakuu wengine, kwanza kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kasha kwa ajili ya dhambi za hao watu, maana yeye alifanya hivi mara moja, alipojitoa nafsi yake.”[8]
 Atakaye kuwa mkubwa na awe mdogo.[9] Katika utumishi wetu tunapaswa kuongozwa na unyenyekevu. Tunapoamua kujitoa kwa ajili ya wengine ili kuwatumikia, hatuna budi kujishusha ili tuweze kuendana na hadhira.
Kuhani ni nani?
Maana kila kuhani mkuu aliyetwaliwa katika wandamu amewekwa kwa ajili ya wandamu katika mambo yamhusuyo Mungu, ili atoe matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi; awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katik ahali ya udhaifu; na kwa sababu hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi. Na hapana mtu ajiywaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni. Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakinii yeye aliyemwambia, ndiwe mwanangu, mimi leo nimekuzaa.”[10]
Tunaambiwa Yesu ameanza kuhubiri au kufundisha yapata miaka kama thelathini.[11]  Nawe je umeanza kufundisha au kumtangaza Kristo katika maisha yako ukiwa na umri gani? Tafakari sasa, ni mara ngapi umeshindwa kutekeleza wajibu wako kama Mkristo? Mara ngapi kama Mkristu umeshindwa kuwasikiliza wale wanaokuja kuomba msaada? Ni mara ngapi umetupilia mbali ombi au misaada ya wanaokulilia uwasaidie?
Hakika utumishi tunaoongelea hapa ni ule wa kutenda na kufanya vitu kwa Upendo kama Kristu alivyotutendea nasi tuliokuwa hatusitahili; ila akatusitahilisha. Kuna mtu mwingine anaweza akawa na vitu fulani vilivyo ndani ya uwezo wake. Lakini ule mguso wa utumishi kwa wote akakosa. Ndipo hapo kwa mfano mtu anakuja kuomba umsaidie hata chakula, na kwa kuwa anajua una chakula tena cha kutosha. Unaishia tu kumpa pole, pale anapokwambia umsaidie kwani amelala njaa. Tusiwe watu wa kuchukulia mambo juu juu tu (sympath); bali watu wa kuvaa shida za wengine na kuziona kama ni zetu yaani zituguse (empanth). Na huu ndiyo utumishi wenyewe, wa kuwa tayari na kuwajibika kwa ajili ya wengine.


SEHEMU YA TATU

MATENDO

3.0 UTANGULIZI

Matendo yanaongea au yanasema zaidi kuliko maneno.  Haya ni maneno ambayo tumeyazoweya kuyasikia mara nyingi. Nitoe mfano mmoja ambao utatupa tafakari nzuri ya kutambua matendo haya ni nini maana yake katika maisha. Walitokea watu wawili walioishi kwa kupendana na kujaliana. Mmoja aliitwa FRIDA na mwingine aliitwa MAUA, yaani walikuwa wameivana sana. Sasa kama tujuavyo hakuna masika isiyo kuwa na ncha, yaani hatuwezi kukaa na kutegemea kuwa mara zote maisha yataenda vile tutakavyo. Sasa ikatokea MAUA akaugua ghafla. FRIDA akapata taarifa kuwa rafiki yake MAUA alikuwa ni mgonjwa basi akaenda kumwona na uzuri alikuwa jirani yake tu hatua kadhaa mpaka kufika kwake. Sasa FRIDA akamshauri MAUA aende kufanya vipimo hospitalini. Kweli akajitahidi kwenda zahanati akapimwa, ila akaambiwa hawajaona ugonjwa wowote ule. Basi akarudi kwanza nyumbani na kuanza kujiapanga ili aweze kwenda kituo cha afya pia kwa vipimo zaidi.
Siku ya siku ameshajiandaa akaenda, pia majibu yakatoka ya kuwa hawaoni tatizo lolote. MAUA akawaza moyoni tatizo ni lipi sasa? Mbona hali inazidi kudhoofika zaidi? Akajisemea moyoni kwa kuwa bado nina kitu mfukoni ya kuniwezesha, ngoja niende hospitali ya Wilaya. Akaunganisha na kufika kule, majibu yakawa yale yale kuwa hawaoni ugonjwa. Basi akaamua kurudi nyumbani na kusema basi bora nikae nymbani tu ili nifie hapa hapa kwa watoto wangu na mume wangu. Sasa baada ya FRIDA kusikia kuwa shahiba wake amerudi kutoka hospitali, basi akasema ngoja akamwone. Kumbuka tuko katika ulimwengu wa utandawazi sasa, cha ajabu na cha kutisha walipenda kuwasiliana sana na wakati mwingine kwa njia ya simu. Hallo... shogaa yangu naomba leo saa kumi kamili unisindikize kusuka saloon. Na hivyo walishirikiana vema, ila maajabu wakati wote yuko huko hospitali hakuthubutu kumtafuta na kumwuliza juu ya maendeleo yake.
Kwa hiyo FRIDA aliposikia amerudi kutoka hospitali alikwenda kumwona MAUA. Alipofika na kumwona alivyokuwa amekonda loo….. hata neno la faraja ya kuwa pole sana shogaa yangu halikutolewa. Mwisho wa siku akaangua kilio na hatimaye wote wawili wakawa watu wa kutoa machozi tu. Basi baadae FRIDA aliinuka na kurudi nyumbani. Hata hakupata tena hamu ya kwenda kumwona rafiki yake…………     Ndugu msomaji wa kitabu hiki, mwandishi anataka kukupa somo hili       
“Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki.” Na Yoshua bin sira anasema, “Wala usisahau kwenda kumtazama mgonjwa, mradi ukifanya hivi utapata kupendwa na watu.”  Kwahiyo, unapomtembelea mgonjwa unabainisha ukweli huu: rafiki katika shida ni rafiki wa kweli. Unapomtembelea mgonjwa mpe matumaini, usimkatishe tamaa wala usimwongezee uchungu, maumivu na huzuni. Mwambie pole na kumpa matumaini ya kuwa utapona.[12]
Ndiyo maana wanasema ‘moyo wenye furaha, una mwili unaohangaika au kuteseka.’ Na hivyo inakamilishwa na methali isemayo ukiona vyaelea ujue vimeundwa. Kumbe tutambue kuwa matendo yetu yanasema zaidi kuliko kingine chote. Kwa mfano; Wewe huwezi kusema unawapenda watu waote, wakati hapohapo tunaona kuna watu unawanyanyasa sana kwa namna mbalimbali. Hii inatendeka zaidi pale unapokuwa umegubikwa na kutawaliwa na majivuno pia kiburi na kujiona wewe ndiye hakuna mwingine. Ndiyo maana Maandiko yanatuambia ya kuwa hatuwezi kujigamba ya kuwa tuna imani, wakati matendo yetu hayaonekani na hivyo yamekufa.[13]
Mtume Petro mwenyewe wakati wa kukamatwa kwa Yesu alimkana Yesu, kama alivyokuwa amekwisha kumwambia kuwa kabla jogoo hajawika mara tatu utakuwa umenikana kama zisemavyo Injili nne (Mt 26:69-75; Mk 14:66-72; Lk 22:54-62; Yn 18:25-27).

3.1 Kwanini Petro anatambulika kwa matendo?


Ø Namna ya uongeaji (Mt 26:73).
Ø Namna ya kutembea kwake (Mt 26:71).
Ø Namna ya mwonekano wake wa ukaaji (Mt 26:69).
Kupitia Mtume Petro anachotufundisha ni kwamba kama msemo mmoja usemavyo kuwa ‘hujafa hujaumbika.’ Na hivyo tunaaswa tuepukane na kujiamini kipumbavu.  Lakini pale matendo yetu yanapoonyesha Ukristo wetu kwa wengine, basi tuwe tayari kuendelea kuwadhihirishia watu hawa kuwa ndivyo tulivyo kama Wakristo. Na pia pale tunaposhindwa kuwa waaminifu katika kuuonyesha Ukristo wetu basi tuwe tayari kutafuta upatanisho kama alivyoanza kulia Mtume Petro. Kwa maana ya kawaida tu kama wanadamu tu dhaifu na hivyo tunapaswa kulipokea hilo na kulifanyia kazi pale tunapoona kweli hatujaenenda vile ipasavyo. “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo, wala neno lake halimo mwetu.”[14]

3.2 Ahadi ni deni


Mwenyezi Mungu ni mwaminifu katika ahadi zake hata ikipita miaka elfu na maelfu, anabaki mtekelezaji mwaminifu.  “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe. Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba. Angalieni, kesheni, (ombeni), kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.”[15]
Ahadi ni kipimo cha kutosha juu ya uaminifu kwa mhusika. Ni kwa mantiki hiyo inapofikia hatua ya utekelezaji tu, hapo mtu anaonekana na kuonyesh ule uaminifu wake kwa kutekeleza ahadi au kile alichoahidi. Lakini sasa bila kubagua, Wakristo walio wengi siku hizi wamekuwa kama wanasiasa ambao ni wepesi wa kusema tu ila utekelezaji unakuwa zero.
Sasa kama Wakristo Wakatoliki tunaweka ahadi zetu kwa Mungu juu ya kumkataa shetani na kuungama imani yetu. Licha ya hulka yetu kama binadamu, kuna wakati tunavunja ahadi hizo ama kwa kutokujua kweli au kwa kujua (tukiwa na uelewa wa kutosha juu ya kile tuanyacho kuwa siyo). Na hii kwa watoto watoto wachanga, wazazi na wasimamizi ndiyo wenye jukumu hili la kusema ahadi hizo kwa mgongo au niaba ya watoto hao. Ila kwa wakatekumeni basi kwa kuwa wanakuwa ni watu wazima, hivyo wanakuwa na uelewa wanajibu pia wao. Au kwa Waamini wote hujikumbushia ahadi hizi siku ile ya mkesha wa Pasaka. Na katika kujibu inakuwa katika nafsi ya kwanza umoja (yaani unajibu wewe kama wewe au kama vile ulikuwa unaulizwa peke yako).

3.2.1 Kumkataa shetani na kuungama imani[16]

Padre anawashauri wazazi na wasimamizi kwa maneno yafuatayo:
Ndugu zangu, wazazi na wasimamizi, watoto mliowaleta karibu watapata uzima mpya utokao katika mapendo ya Mungu, kwa maji na Roho Mtakatifu, kwa Sakramenti ya Ubatizo. Basi, ninyi jitahidini kuwalea katika imani, kusudi uzima ule wa Mungu usichafuke, bali uweze kukua ndani yao, siku kwa siku.
Basi, iwapo kwa imani yenu mko tayari kupokea wajibu huo, mkikumbuka na Ubatizo wenu ninyi wenyewe, kataeni dhambi na kuungama imani katika Yesu Kristu, hiyo ndiyo imani ya Kanisa wanamobatizwa watoto.
Mwamkataa shetani?                                                                                              Wazazi na Wasimamizi  Namkataa.
Na mambo yake yote?                                                                                              Wazazi na Wasimamizi  Nayakataa.
Na fahari zake zote?                                                                                               Wazazi na Wasimamizi  Nazikataa.
Mwasadiki kwa Mungu Baba mwenyezi, mwumba mbingu na dunia?                                                                                              Wazazi na Wasimamizi  Nasadiki.
Mwasadiki kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee, Bwana wetu, aliyezaliwa na Bikira Maria, akateswa, akafa, akazikwa, akafufuka katik wafu, amekaa kuume kwa Baba?                                                                                                                Wazazi na Wasimamizi  Nasadiki.
Mwasadiki kwa Roho Mtakatifu, Kanisaa Tkatifu Katoliki, ushirika wa Watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili na uzima wa milele?                                                                                              Wazazi na Wasimamizi  Nasadiki.       
Hiyo ndiyo imani yetu. Hiyo ndiyo imani ya Kanisa, tunayoona fahari kuiungama katika Yesu Kristu Bwana wetu. Wote Amina.
Kwa hiyo, kama Wakristo Wakatoliki tuna deni la kutekeleza kwa kuishi ahadi zetu za Ubatizo. Ndiyo maana nimekuja na msemo huo kuwa ahadi ni deni.

 

3.2.2 Tu watoto wa Mungu

Mpendwa msomaji wa kitabu hiki, tambua ya kuwa mpaka sasa wewe ni mtoto wa Mungu. Kwani kwa Ubatizo, Mungu ametupokea kama wana wake katika Kristu.[17] Ndiyo maana tunaaambiwa kuwa “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.”[18]

SEHEMU YA NNE

IMANI

4.0 UTANGULIZI

Ingawa kwa Kiswahili neno imani lina maana mbalimbali. Ila zaidi  inahusiana na kitenzi kuamini, kinachofanana na kusadiki. Hapo ni kukubali ukweli wa jambo lisiloweza kuthibitishwa. Katika dini msingi wake ni mamlaka ya Mungu aliyeshirikishwa ukweli huo kwa njia ya ufunuo maalumu ili kumsaidia binadamu amjue yeye, ajifahamu pamoja na maisha yake duniani na ya baadaye. Kwa msingi huo, au wa namna hiyo, mtu anaweza kushikilia jambo bila ya uthibitisho mwingine, ingawa pengine Ukristo unatia maanani pia akili katika ujuzi wa ukweli. Kadiri ya Mtume Paulo imani ikifuatana na tumaini na upendo ni adili kuu mojawapo, msingi, mzizi na chanzo cha wokovu. Na hivyo kwa husrikiana na makala[19] tunaweza kujifunza kwa mapana juu ya imani kama Wakristo.

4.1 Roho ya imani katika maisha ya kiroho

Kila mara mtu anafuata ama umbile, asipopita fikra za kibinadamu tu (Imani), anapolenga mbinguni kwa njia ya utakatifu. Roho hizo zinazotuongoza maishani ni namna maalumu za kupima, kuona, kuhisi, kupenda, kushabikia, kutaka na kutenda. Basi, roho ya imani ni kupima yote kwa mtazamo wa juu ambao unapita maumbile na kutegemea mamlaka ya Mungu katika kujifunua, na ukweli wake katika kutushirikisha utukufu. Tunaelewa zaidi roho ya imani tukiangalia iliyo kinyume chake, yaani upofu wa roho unaozuia mtu asione mambo ya Mungu isipokuwa kidunia na kutoka nje. Ndiyo maana Israeli haikuelewa uteuzi wake kadiri ya ukweli wa Mungu ulio wa juu kuliko ukabila au ubaguzi wowote.
Imani ina mitazamo mipana kuliko hiyo ya Waisraeli,  kutokana na usahili wake unaoshiriki hekima ya Mungu. Kumbe “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.”[20] Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu: kwa kuwa ametushirikisha Roho wake. Imani ni nje ya milango mitano ya fahamu kwa maneno mengine. Juu sana kuliko mifuatano ya mawazo, ni tendo sahili ambalo tunamsadiki Mungu anayefunua na papo hapo anajifunua. Kwa tendo hilo lipitalo maumbile tunaambatana naye pasipo udanganyifu na hivyo katika giza tunalenga kutazama mambo ya Mungu, juu kuliko hakika zote za kibinadamu. Hakika inayotokana na imani tuliyomiminiwa na Mungu, inapita hata hakika ya akili tunayoweza kujipatia kwa kuzingatia miujiza inayothibitisha ufunuo wake.
Imani ni zawadi ya Mungu: “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu.”[21] Ni kama hisi ya Kiroho inayotuwezesha kusikia ulinganifu wa mafumbo aliyotufumbulia, yaani kusikia sauti yake kabla hatujakaribishwa kumuona uso kwa uso.
“Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia bali Roho itokayo kwa Mungu, makusudi tupate kujua tuliyokirimiwa na Mungu, nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Basi, mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu. Maana, ni nani aliyefahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.”[22] Ili ifanye hivyo imani inasaidiwa na vipaji vya akili na hekima, lakini yenyewe ndiyo inayotufanya tushike Neno la Mungu pasipo udanganyifu.
Ingawa mafumbo yake ni ya giza kwetu, adili la imani ni bora kuliko ujuzi mwangavu walionao malaika kwa umbile lao, kwa sababu imani tunayomiminiwa inalingana na uzima wa milele, kwa kuwa ndiyo mbegu yake. Malaika wenyewe walihitaji zawadi hiyo waweze kulenga hali ipitayo maumbile waliyoitiwa. Mungu anapotujalia imani, anapenya roho yetu na kusema nayo si kwa mifuatano ya maneno, bali kwa wazo la ghafla. Imani ikifika, tunaachana na mfuatano wowote wa mawazo tuliokuwanao pamoja na sababu zake: tunaviweka chini ili imani ivikalie kama mtawala. Imani ikiangaza akili kwa mng’ao wa kweli zake, mara utashi unahisi joto la upendo wa Mungu. “Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu. Imani inatakiwa kukua kila siku.”[23]

4.2 Imani tuliyomiminiwa inatakiwa kustawi hadi kifo

Mwito ni huu; “Enyi mnaomcha Bwana, mwaminini Yeye sana, thawabu yenu haitawapotea. Enyi mnaomcha Bwana, sasa tarajieni mema na furaha ya daima na rehema. Angalieni vizazi vya kale mkaone: nani aliyemtumaini Bwana akaaibika? Nani aliyekaa hali ya kumcha akaachwa? Nani aliyemwita akadharauliwa?”[24]  Kumbe,“Imani inaweza ikawa kubwa ndani ya Mkristo mmoja kuliko ndani ya mwingine, upande wa akili kutokana na hakika na imara kubwa zaidi katika kushika ufunuo, na upande wa utashi kutokana na utayari na utiifu au tumaini kubwa zaidi” kwa kuwa; “imani tunayomiminiwa inalingana na zawadi ya neema, ambayo si sawa kwa wote” alisema Mtakatifu Thoma wa Akwino. Yesu Kristo mwenyewe aliwasema wanafunzi wake kuwa wana imani haba[25] ; kumbe alimuambia mwanamke Mkananayo kuwa Mama, imani yako ni kubwa![26]
Imani inaweza kukua kwa upana na kwa dhati au nguvu. Inapanuka tunapozidi kujifunza yale yote Kanisa linayoyafundisha. Kumbe, wanateolojia wanayajua wazi, lakini si kwamba imani yao ni ya dhati na ya nguvu kadiri ilivyoenea. Hivyo, tunakuta watakatifu wasiojua mengi katika hayo, lakini wanapenya mafumbo yalivyofumbuliwa na Injili kwa usahili. Mitume wa Yesu walimuomba imani hiyo waliposema, Tuongezee imani.[27]  Yesu akawaambia, “Yoyote mtakayoomba katika sala mkiamini, mtapokea.”[28]  Tutayapokea hasa tukijiombea kwa udumifu yaliyo ya lazima au ya kufaa sana kwa wokovu wetu, kama vile ustawi wa maadili.

4.3 Ubora na uwezo wa imani

Thamani ya imani inapimwa na matatizo inayoyashinda katika majaribu: “Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu… yeye aliyeambiwa: Katika Isaka uzao wako utaitwa, akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka kuzimu… Kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, walizima nguvu za moto. Wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani; walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizungukazunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi, walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao.” Mambo kama hayo yanatokea hata siku hizi. “Basi na sisi pia, tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu, tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.”[29]
Gregori Mkuu (540-604) alisema, “Mzingatieni Kristo aliyevumilia upinzani wa namna hiyo kutoka kwa wakosefu. Hapo katika tabu yoyote mtaona dawa katika msalaba wa Yesu. Humo mtakuta vielelezo vya maadili yote”. Mtakatifu Thoma wa Akwino (1225- 1274) alisema, “ukiyakumbuka mateso ya Yesu hatutaona chochote kuwa kigumu au cha tabu tusiweze kukivumilia kwa subira na upendo.” Imani ikistawi inatufanya kwa kawaida tuzidi kuhisi fumbo la Kristo; polepole hisi hiyo ipitayo maumbile inakuwa sala ya kumiminiwa yenye kupenya na kuonja, asili ya furaha na amani: “Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, furahini… Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”[30]

4.4 Tuishije kwa roho ya imani?

ü Tunapaswa kuishi hivyo kwa kupima yote kwa mwanga huo wa juu: kwanza Mungu, halafu nafsi yetu, jirani na matukio yote. Je, kuna haja ya kusema tumzingatie Mungu kwa imani? Bila ya shaka! Kwa kuwa mara nyingi tunamzingatia kwa dhana zisizo na msingi, kwa miguso ya kibinadamu mno na kwa maono yetu, badala ya kupitia ushuhuda alioutoa juu yake mwenyewe. Pengine hata tunaposali tunajisikiliza tu kwa kumkopesha Mungu mawazo yetu yanayotokana na umimi. Tunapojiamini kipumbavu tunaelekea kudhani huruma ya Mungu ni kwa ajili yetu, na haki yake kwa watu tusioelewana nao. Kumbe tukikata tamaa tunatilia shaka kimatendo upendo wa Mungu kwetu na huruma yake kuu. Kwa imani tunamuona Mungu kupitia mafumbo ya maisha na mateso ya Mwokozi na kupitia uhai wa Kanisa linalofanywa upya na Ekaristi Takatifu tuipokeayo kila siku.

ü Jicho la imani linasifika zaidi na zaidi kwa ufishaji wa hisi na maono, maoni na matakwa yetu: hapo tu unakuja kuanguka polepole ule mtaji wa kiburi na majivuno unaotuzuia tusione mambo ya Mungu au tuone tu vivuli vyake na tata zake.
ü Tunapaswa vilevile kujitazama kwa imani. Tukijitazama kibinadamu tu, tunaona ndani mwetu sifa za umbile ambazo mara nyingi tunazizidisha. Baadaye, majaribu yakituonyesha tulivyojidanganya tunavunjika moyo kwa urahisi. Kumbe kwa imani tunakuja kujua utajiri upitao maumbile ambao Bwana ametutia katika ubatizo na kutuongezea kwa Ekaristi Takatifu, yaani thamani ya Neema inayotia Utakatifu, ya uwemo wa Utatu Mtakatifu pamoja na Ukuu wa Wito wa Kikristo. Tunakuja kujua pia vizuio vya ustawi wa uzima huo, kwa mfano usahalifu wa mbegu ya uzima wa milele iliyopandwa ndani mwetu, na kiburi cha kipumbavu. Kwa mtazamo huo wa juu tunakuja kujua mapema kilema kinachotutawala na kivutio maalumu cha neema tulicho nacho, ambavyo cha kwanza kikomeshwe na cha pili kistawishwe.
ü Lakini NENO la Mungu linatupa uhakika wa imani kwa kuwa “imani huja kwa kusikia Neno la Kristo.[31] Mtu akiliamini neno la Mungu, kwamba Mungu hawezi kusema uwongo, moyo wake utapokea uhakika huo wa imani). Ndani yake, litajengeka taraji la kupokea, kila anapotoa. Atajua kuwa kutoa sadaka si kupoteza, bali ni kupanda kwa ajili ya mavuno na baraka kutwaa zaidi. Kuanzia sasa, pokea uhakika kwamba, ukitoa kwa imani ya kupokea, utapokea. Ukitoa bila imani ya kupokea, hautapokea, utakuwa umechangia tu. Hivyo mbegu haiwezi kuzaa, kwa maana “….kila tendo lisilotoka katika imani, ni dhambi.”[32]

ü Hakuna mkulima anayeweza kutoa kidogo, wakati anaamini mavuno ni mengi. Atoaye kidogo hana imani ya kupokea. Anaamini inapotea na ndiyo maana anaona ni bora apoteze kidogo.  Lakini mwenye imani ya kupokea, hutoa kwa wingi kwa sababu anajua sadaka yake haipotei, bali imepandwa na itazaa sana. Kutoa sadaka pungufu ya ile uliyoazimia mwanzo au pungufu ya ile aliyokuongoza Mungu kutoa.[33] Ukipanga moyoni mwako kutoka nyumbani kumpa Mungu kiasi fulani cha sadaka, baada ya azima hiyo Mungu anakuwa ameipokea sadaka tayari. Wakati wa utoaji, usipunguze. Laa! sivyo utakuwa unamwibia Mungu. Watu wengi hukosea kwa kufika Kanisani wakiwa wamepunguza sadaka ya Mungu. Katika sadaka hiyo hiyo ananunua gazeti, pipi, au analipa nauli.
    
ü Lakini tunayesahau zaidi kumtazama kwa imani ndiye jirani. Tunamtazama kibinadamu tu, tukiathiriwa na dhana zisizo na msingi, kiburi, wivu na vilema vingine. Kwa hiyo ndani yake tunakubali yale ambayo yanatupendeza kibinadamu, yanatufaidisha au kutukuza; kumbe tunahukumu yale ambayo yanatukinaisha, yanamfanya bora kuliko sisi na kutushusha. Dhambi ngapi za kuhukumu na kusingizia zinatokana na mtazamo huo uliofunikwa na utaji wa umimi! Tukijifunza kumtazama jirani kwa imani ni faida kubwa pande zote. Hapo tunakuja kuwaona wakubwa wetu kama wawakilishi wa Mungu, na kuwatii kwa moyo pasipo kuwasema. Tunaona kuwa wasiotupendeza wamekombolewa kwa damu ya Kristo, pengine ni viungo vya mwili wake vinavyokaribia moyo wake kuliko sisi: mara nyingi tunaishi miaka pamoja na watu safi tusitambue uzuri wa roho zao. Vilevile, tukija kuwatazama kwa imani wanaotupendeza, pengine tunavumbua wana maadili ya Kimungu kiasi cha kuzidisha na kutakasa mapendo tunayowaonea; pia kwa wema tunaona vizuio walivyonavyo kwa utawala wa Mungu na tunaweza kushauriana nao tusonge mbele katika njia yake.

ü Hatimaye tunapaswa kutazama kwa imani matukio yote ya maisha yetu, ya furaha na ya uchungu vilevile. Mara nyingi tunaridhika kuyaona upande wa hisi tu, au kwa akili iliyoathiriwa na dhambi. Mara chache tunayazingatia Kimungu, kwa kuona kwamba “katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema”[34] :hata katika upinzani, matatizo makubwa yasiyotarajika na dhambi (tukiweza kujinyenyekesha kutokana nazo). Katika kukosewa haki na watu tunaweza kutambua haki ya Mungu ikiadhibu makosa ya siri ambayo hatulaumiwi na mtu; au tunahisi majaribu ya Kimungu, na utakaso unaokusudiwa kupatikana kwa njia ya hayo.

ü Kabla ya imani yetu kutakaswa kwa majaribu kadhaa ya aina hiyo, tujitahidi kukua katika imani, badala ya kupima yote kibinadamu tu. Ni lazima tujinyime mianga midogo na ya bandia ili tujaliwe ile ya juu; tuache kufuata mno akili yetu ili tuone uangavu mkuu wa mafumbo ya imani na kuishi kulingana nayo. Hivyo tunaelewa kwa nini hatutakiwi kuitikia vishawishi dhidi ya imani, bali kuvikataa au kuviruka kwa kukiri imani kwa dhati zaidi; Bwana anaviruhusu kwa maendeleo yetu tu.


Tujifunze imani aliyokuwa nayo Petro ambaye baada ya kukesha usiku kucha akivua na hakupata chochote. Na kama ilivyo kawaida ya wavuvi, kazi hiyo inafayika usiku. Lakini licha ya kutambua na kuwa na uzoefu wa kazi hiyo ambayo alikuwa akiifanya, Bwana Yesu Kristo anapofika pale na kumwambia azitupe nyavu zake na kutweka mpaka kilindini basi alitekeleza vema. Kilichomsukuma ni ile imani tu aliyokuwa nayo, ndiyo maana anakubali kwa kusema ‘kwa neno lako nitazishusha nyavu.’[35]
Imani inaenda sambamba na matendo tu. “hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria,bali kwa imaniya Kristo Yesu,sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.” Gal 2:16


SURA YA TANO

SAKRAMENTI NI NINI?

5.0 UTANGULIZI

Kuna namna mbalimbali zinazotufanya kukutana na Kristo Yesu; ambazo ni katika sala, kati ya wenzetu, katika Kanisa, katika kusoma Biblia, kusikiliza neno la Mungu na hasa katika Misa Takatifu na Sakramenti (Rejea Mt 18:20; 25:31-36; Mdo 9:3-6; 2Tim 3:14-17). Basi mpenzi msomaji wa kazi hii nikualike kutafakari nami juu ya Sakramenti. Sakramenti ni alama ya kuwepo kwa Yesu tayari kutuokooa, yaani kutupatia uzima kwa Roho wake. Tunavyozidi kumwamini, ndivyo naye anazidi kutujalia uzima. Kuna jumla ya Sakramenti saba katika Kanisa na ziliwekwa na Kristo mwenyewe; Ubatizo, Kipaimara, Ekaristi Takatifu, Kitubio, Mpako wa Wagonjwa, Daraja Takatifu ya Upadre na Ndoa.
Sakramenti ni ishara ionekanayo wazi ya neema isiyoonekana iliyowekwa na Yesu Kristo ili ilete neema au kuongeza neema rohoni. Sakramenti hizo saba zinagusa hatua zote na nyakati zote muhimu za maisha ya Mkristo. “Sakramenti zinayajalia maisha ya imani ya Mkristo, kuzaliwa na kukua, kupona na utume. Katika jambo hili kuna ufanano fulani kati ya hatua za maisha ya kawaida na hatua za maisha ya kiroho.”[36]
Kuna Sakramenti zinazotolewa mara kwa mara au mara nyingi (Ekaristi Takatifu, Kitubio, Mpako wa Wagonjwa na hata Ndoa), lakini pia kuna zile zinazotolewa mara moja tu katika maisha ya Mkristo (Ubatizo, Kipaimara, Daraja Takatifu ya Upadre).[37] Lakini zifuatazo ni sakramenti ambazo zinatumika kumwingiza mtu katika Ukristo na kumfanya kuwa mdumifu katika misingi ya maisha ya Kikristo ni; Ubatizo, Kipaimara na Ekaristi Takatifu.
Sakramenti ni za Kanisa kwa namna mbili “kwamba zipo kwa njia yake’’ na “kwa ajili yake’’. Ni “kwa njia ya Kanisa’’ kwa sababu Kanisa ni sakramenti ya tendo la Kristo anayetenda ndani yake kwa njia ya utume wa Roho Mtakatifu. Na pia ni “kwa ajili ya Kanisa’’ kwani ndizo sakramenti zinazolifanya Kanisa libaki katika Muungano na Kanisa la mbinguni katika maadhimisho yake hususani katika Adhimimisho la Ekaristi Takatifu; kwani zinadhihirisha na kuwasilisha kwa watu, hasa katika Ekaristi, fumbo la ushirika wa Mungu ambaye ni upendo, mmoja katika Nafsi Tatu.  Sakramenti zimewekwa ili kuwatakatifuza wanadamu. Na ni katika kupokea Sakramenti, mwili wa Kristo unajengwa. Na hivyo Kanisa linasisitiza jumuiya ya waamini wakristo wazifahamu Sakramenti na nguvu katika maisha ya Mkristo.[38]
Sakramenti za Kanisa ni mwalimu tosha, kwani zinawafundisha waamini katika maadhimisho mbalimbali katika Liturujia. Siku zote, Sakramenti zinadai imani thabiti katika kuzipokea. Na mtu anazidi kuimarishwa katika ufuasi wa Kristo pale anapokuwa rafiki wa Sakramenti mbalimbali. Kanisa siku zote linaisisitizia jamii ya waamini wawe na tabia njema ya kupokea Sakramenti mara kwa mara kwa ustawi wa maisha yao kwa utakatifu. Unapaswa kupokea sakramenti huku umeweka lengo na kusudi la kuipokea sakramenti hiyo kwa ajili ya kujitakatifuza.[39] Sakramenti tuzipokeazo zitufae kwa wokovu wetu. Kama tutazipokea kwa lengo jingine au pasipomastahiri yetu kama hatujajiandaa kiroho.Tutakuwa tunapoteza muda na tunacheza mchezo wa kuigiza tu.Kwani tujikuta tunapokea sakramenti mara dufu bila kuchota neema zozote zitokanazo na sakramenti hizo.
Hivyo basi, Sakramenti ni kwa ajili ya kutakatifuza waamini wakristo.Sakramenti ni muhimu sana kwa wokovu.Wokovu huo ni wakuwafikisha uzima wa milele. Katika Sakramenti zote Roho Mtakatifu anahusika moja kwa moja, Kwani Roho Mtakatifu ni Mungu aliye sawa na Baba na Mwana. Sakramenti zote zinaangazwa na kuimarishwa na Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu na   Fumbo zima la Utatu Mtakatifu wa Mungu hujidhihirisha katika Maisha ya Mkristo kwa njia ya Sakramenti mbalimbali. “Roho Mtakatifu huwaandaa waamini kwa Sakramenti kwa njia ya Neno la Mungu na kwa njia ya imani inayolipokea Neno hilo katika mioyo iliyo tayari. Kwa hiyo, sakramenti huimarisha na kuonesha imani.”[40]
Ni kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo tunakuwa watoto wa Mungu. Tunaondolewa dhambi ya asili na dhambi nyingine.Tunakuwa jamii ya waamini wa Yesu Kristo.Na kwa Sakramenti ya Ekaristi Takatifu, Sakramenti hii ina nafasi ya pekee kwa kuwa ni “Sakramenti ya Sakramenti’’: nyingine zote zimeelekezwa kwa Ekaristi kama lengo lao.[41] Tunampokea Yesu Kristo katika Maumbo ya Mkate na Divai, mapaji ya Mkate na Divai hugeuzwa kuwa Mwili na Damu ya Kristo baada ya Mungu Baba kuwa amemtuma Roho Mtakatifu aweze kuvitakasa vipaji hivyo (Mkate na Divai ) ili viwe Mwili na Damu kweli ya Kristo. Hayo hufanywa katika adhimisho la Misa Takatifu ambapo, Padri kwa kumsihi Mungu Baba aweze kugeuza Mkate na Divai kwa kumtuma Roho Mtakatifu (Epiklesis). Hivyo basi, hakuna Misa Takatifu bila adhimisho la Ekaristi Takatifu. Ekaristi takatifu ndiyo Kiini cha Maisha ya Kanisa Katoliki, kwani ndiye Kristo jana leo na milele yote.
Sakramenti ya Kitubio, kwa kujipatanisha na Mungu na jirani zetu; tunajipatia neema mbalimbali na hayo yanafanywa kwa kuungama dhambi zetu. Sakramenti ya Kitubio hutupatanisha na Mungu na jirani zetu pia.Tunarudisha urafiki wetu kwa Mungu kwa njia ya Sakramenti ya Kitubio.Kitubio ni  dawa ya dhamiri zetu.Kitubio hutuponya majeraha tuyapatayo katika  maisha yetu.Kitubio ni ishara ya unyenyekevu na kujikubali mbele ya Mungu na kuhani wake  yaani Padre kuwa tuwadhambi na tukiungama tutasamehewa dhambi zetu.
Sakramenti ya Kipaimara hutuimarisha katika kuutetea ukristo wetu kwa gharama zozote,kufa ikiwa lazima,imani Katoliki ibaki salama.Ni kwa Sakramenti ya Kipaimara tunampokea Roho Mtakatifu mara ya pili anayetutajirisha kwa vipaji mbalimbali vya Roho Mtakatifu kama, :  i.Hekima  ii. Akili iii.Shauri iv.Nguvu v.Elimu vi.Ibada vii.Uchaji wa Mungu.
Mpako wa  wagonjwa ni sakramenti inayomtia nguvu Mkristo aweze kuyapokea maumivu na shida katika magonjwa yake kwa kumtumainia Yesu Kristo aliye Mwokozi wetu na mfano halisi wa Mungu Mtu aliyepata mateso makali ,ni nani atakayeyasimulia?.Sakramenti ya mpako wa wagonjwa huweza kumponya Mkristo Kiroho zaidi na kimwili pia.
Sakramenti ya Ndoa ,ni muungano  wa mwanaume na mwanamke katika kuendeleza kazi ya Mungu ya uumbaji, Kuishi pamoja kwa maisha yao yote.Ni muungano katika Uaminifu unaofaidisha ustawi wa wanandoa wenyewe wafurahie maisha yao ya ndoa na watoto watakaowapata wawalee Kikristo.Ni muungano unaofanywa mbele ya shahidi rasmi wa Kanisa yaani  Shemasi ,Padri au Askofu Mkatoliki.Na hivyo hufanywa kuwa Sakramenti.
Waadhimishaji wa Sakramenti ya Ndoa ni wahusika wenyewe yaani Mume na Mke baada ya Maridhiano yao.[42] Ndoa Katoliki haivunjwi kwa mamlaka yoyote duniani , Ndio maana,  Moja ya sifa ya Ndoa Katoliki ni  Umoja, na  Uimara wa ndoa (Kudumu kwa ndoa mpaka kifo kiwatenganishe).[43] Na ni kwa vigezo hivyo, Ndoa Katoliki huwa Sakramenti.
Sakramenti ya Upadrisho, Daraja Takatifu au Upadre ni Sakramenti inayompa mwanaume mkatoliki uwezo mtakatifu ili :Atolee sadaka ya Misa Takatifu, Awashirikishe watu sakramenti na Awahubirie na kuwafundisha watu rasmi (Rej. Eb 5:1-4; 1Kor 11:24-25), Pia Awaongoze watu na kutoa baraka (Rej. KKK Na.1592 na Na.1598).[44] Maisha yetu ya ukristo yanajikita katika kupata Sakramenti Mbalimbali za Kanisa.
Hivyo basi, maisha ya Mkristo na yanaongozwa na Mungu wa Utatu Mtakatifu; katika kupokea sakramenti mbalimbali za Kanisa kwa ajili ya wokovu wa roho zetu.          

5.1 SAKRAMENTI YA UBATIZO

Sakramenti hii huitwa  Ubatizo kutokana na madhehebu ya msingi ambayo kwayo yanafanyika; tendo  la kubatiza  kwa Lugha ya Kigiriki ni  baptizein likimaanisha  ‘’Kutumbukiza’’ au ‘’Kuzamisha’’ ndani ya maji, ndiyo kama alama  ya maziko ya mkatekumeni katika kufa  na Kristo na kufufuka pamoja naye pia. Baada ya hapo anakuwa kiumbe kipya. Anayebatizwa anauvua utu wa kale anauvaa utu upya na kujinyakulia sifa ya kuwa kiumbe kipya Mwana wa Mungu. Anayebatizwa anaingia katika orodha ya watoto na taifa la Mungu. Hivyo basi ubatizo ndio mlango wa Sakramenti zote yaani ndio lango la kuingilia uzima katika Roho. Kwa njia ya Ubatizo tunafanywa huru toka dhambi na tunazaliwa upya na kuwa watoto wa Mungu, tunakuwa viungo vya Kristo na tunaingizwa katika Kanisa na tunafanywa washiriki katika utume wake: Ubatizo ni Sakramenti ya kuzaliwa upya kwa maji katika neno.[45]
Tunampokea rasmi Roho Mtakatifu kwa mara ya kwanza tunapopata Sakramenti ya Ubatizo. Kanisa Katoliki linaamini, linaishi na kufundisha kuwa Ubatizo ndio njia ya kipekee kwa kujipatia wokovu. Kwani Ubatizo ndio mlango wa Sakramenti zote, ndio lango la kuingia katika maisha ya Roho Mtakatifu.[46] Na Sakramenti ya Ubatizo inamtaja na kumfunua Mungu Mmoja katika Utatu Mtakatifu.Hivyo basi ndio maana anayebatizwa anaambiwa, (fulani) Nakubatiza kwa jina la Baba na la Mwana  na la Roho Mtakatifu.[47] Ndio Kanuni halali na yakufaa inayotumika katika Kanisa  Katoliki, inatumika kwani ndio tulioachiwa na Yesu mwenyewe mwanzilishi wa Kanisa hili  Moja, Takatifu, Katoliki na la Mitume. Ndiyo maana tunaithamini Kanuni au fomula ya Ubatizo. Yesu Kristo aliwaambia “Basi nendeni, mkayafanye mataifa yote kuwa wafuasi mkiwabatiza kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.”[48]
Sakramenti ya Ubatizo ni mlango wa sakramenti zote, ni muhimu  sana  na kigezo  mahususi kwa namna ya pekee kwa ukombozi: Iwe kwa kuipokea au kwa kuitamani sakramenti hiyo. Kwa Sakramenti hiyo watu wanaondolewa dhambi zao hususani dhambi ya asili, wanazaliwa upya na kuwa wana wa Mungu na wanafananishwa na Kristo kwa alama isiyofutika, wanaingizwa Kanisani.
Ubatizo unakuwa halali tu, pale katika adhimisho la Sakramenti ya ubatizo Maji yanapotumika kwa kumimina maji kichwani mwa mbatizwa kwa kutumia maneno yanayopaswa kutumia kadiri ya Kanuni maalumu ya Adhimisho la Sakramenti ya Ubatizo yaani fulani (unataja jina la anayebatizwa). Nakubatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu amina.[49] Katika Sakramenti ya ubatizo tunampokea rasmi Roho Mtakatifu katika “Utatu Mtakatifu” na kwa tendo hilo tunajinyakulia hadhi ya kuitwa wana wa Mungu, kwani Mungu ametuzaa rasmi katika Ubatizo huo na Mungu.
Mungu aliyetupatia akili kumjua na utashi wa kumkubali na kuwa naye maishani. Huu ni ukweli ambao dini zote zinazomwabudu Mungu wa kweli hufundisha. Kwa msaada wa Mungu, mwanadamu anaweza kupata ufahamu wa Mungu kupitia akili yake ya kibinadamu. “Na mitume waliokuwako Yerusalemu waliposikia ya kwamba Samaria imekubali neno la Mungu, wakawapeleka Petro na Yohane; ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu; kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa Jina lake Bwana Yesu. Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu (Mdo 8:14 -17)”[50]

5.1.1 Ubatizo wa watoto wadogo

 “Kwa kuwa wanazaliwa na hali ya kibinadamu iliyoanguka na kuchafuliwa na dhambi ya asili, hata watoto wachanga wana lazima kuzaliwa upya katika ubatizo, ili wawekwe huru na nguvu za giza na kuingizwa katika utawala wa uhuru wa watoto wa Mungu, ambao watu wameitwa.”[51]  Watoto wanabatizwa kwa imani ya Kanisa kupitia kwa wazazi wao na malezi ya Kikristo watakayopata tangu Kanisa la kwanza yaani nyumbani mwa Mkristo. Ubatizo wa watoto wadogo umekuwepo tangu zamani.[52] Kwani tangu kale Wakristo wa Kwanza walipokuwa wanafanya zoezi hili la ubatizo inajidhihirisha kuwa hata watoto wadogo nao walijumlishwa katika zoezi la kubatizwa.
Sakramenti ni tendo la Kikanisa, hivyo basi kwa busara ya Kanisa Katoliki inasisitiza ubatizo wa Watoto. Watoto wanaozaliwa nao wapate haki hiyo ya kuitwa wana wa Mungu kwa kutakaswa dhambi zao za asili. Wazazi wanatambua majukumu yao ya kuwalea watoto Kikristo kwa kuwasaidia na kuwatunza kiroho na kimwili. Kuwaongoza maisha mema ya kiuadilifu nay a upendo kwa Mungu na jirani.

5.1.2 Na kuhusu watoto waliokufa bila kupata Ubatizo

Upendo wa Mungu siku zote hauna mipaka. Vilevile, hapendi hata mmoja wetu apotee. Kwa sababu ya upendo wa Mungu kwa Mwanadamu Kanisa linaweza tu kuwakabidhi kwa huruma ya Mungu, kama linavyofanya katika madhehebu ya mazishi yao. Kwani ni kwa huruma ya Mungu na upendo wake iliyomfanya Bwana wetu Yesu Kristo; aseme Waacheni watoto wadogo waje kwangu msiwazuie.[53] Hayo yanatutumainisha kwamba kuna njia fulani ya wokovu kwa ajili ya watoto wachanga wanaokufa bila ubatizo. Na ndio maana Kanisa haliwazuii watoto kupata Sakramenti. Kwani tunaambiwa na Mama Kanisa Katoliki kuwa Mtu yeyote ambaye hajabatizwa ndiye pekee anayeweza kubatizwa.[54]

 

 

5.1.3 Ubatizo unatuingiza katika Fumbo la Ukombozi

Ubatizo ni Sakramenti inayotushirikisha fumbo la Pasaka, ndilo umbo la Ukombozi wetu, la Kufa na Kufufuka kwake Kristu. Tendo lenyewe la Ubatizo laonyesha hiyo, hasa mtoto au mtu mzima (Wakatekumeni) akizamishwa majini. Hamfahamu ya kuwa sisi sote tulibatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya Ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.[55]

Tunapozamishwa majini tunaunganishwa na Kristu katika kifo chake na kuondolewa dhambi; tunapotoka majini tunaunganishwa naye katika ufufuko wake, tunajaliwa uzima wa milele. Ni katika ubatizo tunaondolewa dhambi zetu zote kwa nguvu ya Msalaba wa Kristu; tena tunayakataa kabisa maovu yote na kuyazika maisha ya kipagani, tusije tukafanya dhambi tena. Kasha, tunatoka majini tumejaa uzima mpya tumefufuka pamoja na Yesu na kushika mwenendo mpya wa kikristu na kuishi kwa ajili ya Mungu.[56]

5.2 SAKRAMENTI   YA KIPAIMARA

Kipaimara ni Sakramenti inayotuletea Roho Mtakatifu na mapaji yake ili kutufanya wakristo imara na askari hodari wa Yesu Kristo hata tuweze kushuhudia imani yetu kwa maneno na matendo.[57] Kipaimara hukamilisha neema ya ubatizo; ni sakrament inayomtoa Roho Mtakatifu kwetu ili kututia mizizi ya kina kwa uthabiti zaidi Katika Kristo. Huufanya muungano wetu na Kanisa uwe wenye nguvu zaidi, hutuhusisha kwa karibu zaidi na utume wake na hutusaidia kuishuhudia imani kwa maneno yanayofuatana na matendo. Wakati wa Sakramenti ya Kipaimara, paji la Roho Mtakatifu linaimarishwa ndani mwetu na linatubidisha kuwa na moyo wa kutumikia jirani zetu na kutetea Mafundisho ya Kanisa Moja, Takatifu, Katoliki na la Mitume, na kubaki Imara bila kutetereka katika kutetea Imani yetu ya Kikristu.
Ni kwa Sakramenti ya Kipaimara Kanisa linatuimarisha na kututaka tuipokee Imani ya Kanisa Katoliki kiutu uzima, bila Mchezo! Na hivyo basi, kila mmoja anapaswa aishi kama “nuru” au mwanga aweze kuangaza kati ya jirani zake na kutumia karama kwa faida ya wote, na kuonesha amekomaa katika Ukristu na anayafanyia kazi yale Kanisa Katoliki linayoyafundisha kwani siku zote kanisa letu katoliki linafundisha kwa msaada wa Roho Mtakatifu ambaye ndiye “kingo” au nguzo “msingi” na msimamizi mkuu wa shughuli zote za Kanisa katika kuinjilisha ulimwengu wote (Rej. Papa John Paul II). Watu wote wapate kumjua Yesu Kristu. Kila goti litapigwa na kila ulimi utakiri kuwa Yesu Kristu ni Bwana.
Sakramenti ya Kipaimara huweka chapa isiyofutika sawa na ile ya ubatizo,chapa hiyo isiyofutwa huwekwa ndani ya Roho ya Mkristo alama ya kiroho au muhuri usiofutika, kwa sababu hiyo sakramenti hii hupokewa mara moja tu katika maisha. Inasema, Kanisa la Mashariki, wao ni tofauti na Kanisa letu hili la Kilatini, wao huadhimisha Sakramenti kwa watu mara baada ya ubatizo na hufuatwa na ushirika katika Ekaristi, mapokeo ambayo huonesha wazi umoja wa sakramenti hizi tatu za kuingizwa katika Ukristo.
Katika Kanisa letu hili la Kilatini, Sakramenti hii hutolewa kwa yule aliyetimiza umri wa kuweza kutumia akili, nayo imehifadhiwa iadhimishwe, kwa kawaida na askofu kuonesha kwa namna hiyo kwamba sakramenti hii huimarisha vifungo vya kikanisa. Mwanafunzi wa Kipaimara, aliyetimiza umri wa kutumia akili hutakiwa kuungama imani, awe katika hali ya neema, awe na nia ya kupokea sakramenti na kuwa tayari kuchukua nafasi yake ya mfuasi na shahidi wa Kristo katika umoja wa Kanisa na katika malimwengu.[58]
Madhehebu ya lazima ya Kipaimara ni mpako kwa Krisma takatifu katika paji la uso wa mbatizwa (Kwa Kanisa la Mashariki: pia juu ya viungo vingine vya milango ya fahamu), pamoja na kuwekewa mkono wa mhudumu na pamoja na maneno:  Accipe signaculum doni Spiritus Sancti) (Pokea  muhuri wa paji la Roho Mtakatifu) katika madhehebu ya kirumi; na (Signaculum doni Spiritus Sancti)  “muhuri wa paji la Roho Mtakatifu’’)katika madhehebu ya Byzantina.[59] Kipaimara kinapoadhimishwa kwa kutenganishwa naUbatizo, muungano wake na Ubatizo huoneshwa, miongoni mwa namna nyingine, kwa kurudia ahadi za ubatizo. Adhimisho la Kipaimara wakati wa adhimisho la Ekaristi huonesha mkazo wa umoja wa sakramenti za kuingizwa katika Ukristo.[60]
Pengine Sakramenti hii ya Kipaimara inaweza ikatolewa kwa mtu wakati wa hatari ya kifo kama alikuwa bado hajapata Sakramenti hii maanake ikafuatana na Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa. Sakramenti ya Kipaimara ni ishara ya ujio wa Roho Mtakatifu, ndani ya mtu kwa hali isiyo ya kawaida. Sakramenti hiiimedhamiria kuwapa Wakristo wa kawaida kuonja matukio yale ambayo wanafunzi wa Yesu waliyapata siku ya Pentekoste. Ujio wa Roho Mtakatifu unamjaza mtu ari ya kukiri imani yake hata wakati anapopata vipingamizi vyenye mateso makali vya kumwondoa katika mkono wa Mungu, kama ilivyokuwa wakati wa dhuluma.
Sakramenti ya Kipaimara humfanya mkristo ajazwe na Mapaji Saba ya Roho Mtakatifu kama Kanisa linavyofundisha. Mapaji saba ya Roho Mtakatifu anayopokea  Mkristo katika Sakramenti ya Kipaimara ni:  i. Hekima  ii. Akili iii. Shauri iv. Nguvu v. Elimu vi. Ibada  vii. Uchaji wa Mungu
Sakramenti ya Kipaimara inawaimarisha Wakristo kukabiliana na misukosuko ya kiimani, ,kutangaza Enjili hata katika maeneo na nchi zenye vipingamizi na ukanwaji wa Ukristo,kupokea mateso kwa utulivu kutoka mikononi mwa Mungu, na kuishi kulingana na wajibu wake kama mzazi, afisa, mwajiriwa, jirani au katika nafasi nyinginezo.
Katika Sinodi ya kwanza Jimbo Katoliki Kigoma (25 Mei, 2006 -1 Oktoba, 2011) ilisisitizia juu ya Sakramenti ya Kipaimara kuwa ‘’Yawepo pia Mafundisho endelevu baada ya Kipaimara hadi hatua ya kupokea sakramenti ya ndoa. Mafundisho hayo yatawahusu pia wale waliobatizwa katika utu uzima.

5.2.1 Sheria za Kanisa Katoliki juu ya Sakramenti ya Kipaimara

Sakramenti ya Kipaimara inampatia Mkristo   muhuri, kwa hilo  wabatizwa wanaendelea na njia ya kuingizwa Ukristo. Wanatajirishwa na paji la Roho Mtakatifu na wanajishikamanisha na Kanisa. Wanaimarishwa katika Imani na kupaswa kuwa mashahidi wa Kristo kwa kutangaza na kuilinda Imani kwa maneno na matendo yao.[61]
Sakramenti ya Kipaimara inaadhimishwa kwa kupakwa  Mafuta ya Krisma(Chrism)  kwenye paji la uso wao na kuwekewa  mikono na kwa maneno yanayotambulika kulingana na mwongozo unaotambulika na mamlaka yenye kuonesha maadhimisho ya Sakramenti hiyo.[62]
Krisma (Chrism) inayotumika katika adhimisho la Sakramenti ya Kipaimara lazima yawe yamebarikiwa na Baba Askofu katika adhimisho maalum la Misa Takatifu. Hata kama Sakramenti hii ya Kipaimara inaadhimishwa na Padre, Mafuta ya Krisma (Chrism) yanayotumika ni yale yaliyobarikiwa na Askofu katika adhimisho la Misa Takatifu maalum.[63]
Askofu  katika Jimbo lake anatoa Sakramenti ya Kipaimara kisheria hata kwa waamini wasiokuwa wa Jimbo lake, labda kama itakuwa imeelezwa katazo  kutoka kwa Askofu wao wa Jimbo.[64]
Ili adhimisho la Sakramenti liadhimishwe kisheria katika Jimbo jingine,labda wawe ni waamini wake,Askofu anahitaji apate ruhusa,walau ikiaminiwa na Askofu wa Jimbo.[65]
Padre mwenye uwezo wa kuadhimisha  Sakramenti ya Kipaimara anaweza kupewa idhini  ya kutoa sakramenti ya kipaimara katika eneo  maalum  alilopewa kisheria na lenye kuwa na mpaka alihudumie, hata kwa wale wanaotoka nje ya eneo lile aliloruhusiwa kisheria anaruhusa ya kuwapatia Sakramenti hiyo. Labda kama ikiwa tu, kuna katazo kutoka kwa Askofu wao au Wakili wa Askofu wao (kama Vicar General).Hawezi, hata hivyo kutoa huduma kihalari kwenye eneo jingine, labda kama ametimiza masharti ya Sheria ya Kanisa namba 883, Ibara 3. Inayosema, Wafuatao wanauwezo kisheria, kuadhimisha Sakramenti ya Kipaimara.
1. Katika eneo mahususi ambalo ana uwezo wa kisheria, wale ambao wanaweza kuhudumu  Sakramenti hiyo kisheria wanapata nguvu ya kisheria  na kuwa sawa na Askofu katika adhimisho hilo la Sakramenti ya Kipaimara.
2.  Kwa kuwa Padre, kwa minajiri kwamba ni Padre(ana nguvu za Kikrelo/ Kikuhani  au kwa ruhusa aliyopewa Kisheria na Askofu Jimbo, anayebatiza  au kuwapokea watu wazima katika umoja kamili wa Kanisa Katoliki.
3. Katika hatari ya Kifo, Paroko au Padre yeyote. Maelezo ya Ibara toka Katekisimu bila kubadirisha maana ya sheria hii, bali kupanua ugo wa kuielezea, Kama Mkristo yu katika hatari ya kufa, kila kuhani anaweza kumpa Kipaimara.
Walau mimi mwenyewe mwandishi wa Kitabu hiki nimewahi kushuhudia matukio mawili yanayojikita katika sheria hiyo. Padre aliweza kutoa sakramenti ya kipaimara tukiwa zahanati fulani ambapo mgonjwa maisha yake yalikuwa yanaelekea kumaliza muda wake hapa duniani. Kwa kweli Kanisa hutamani kila mmoja wa watoto wake, hata wadogo wa mwisho, asitoke duniani hapa bila kukamilishwa na Roho Mtakatifu kwa paji la utimilifu wa Kristo.
Inashauriwa kwamba Sakramenti ya Kipaimara iadhimishwe Kanisani wakati wa Misa Takatifu. Hata hivyo, kwa sababu ya haki na ya msingi, inaweza ikaadhimishwa mahali pengine nje ya Misa na katika eneo linalofaa.[66]
Katika Madhehebu ya Kilatini, Mhudumu wa Kawaida wa Kipaimara ni Askofu. Ikiwa ni lazima askofu, anaweza kuwapa mapadre idhini kutoa sakramenti ya Kipaimara.[67] Ingawa inafaa kutokana na maana yenyewe ya Sakramenti, aitoe askofu mwenyewe, ikikumbukwa kwamba kwa sababu hiyo adhimisho la sakramenti ya Kipaimara, mintarafu muda, limetenganishwa na ubatizo. Maaskofu ni waandamizi wa mitume, wao wamepokea utimilifu wa Sakramenti ya daraja. Adhimisho la sakramenti hii linapofanywa na Maaskofu huonyeshwa wazi wazi matokeo ya kuwaunganisha wale wanaoipokea kwa ndani na Kanisa, na vyanzo vyake vya kitume na utume wake wa kumshuhudia Kristo.[68]
Mwadhimishaji   Rasmi wa Sakramenti ya Kipaimara ni Askofu. Padre anaweza pia kihalari kuadhimisha sakramenti hii, ana uwezo wa kuadhimisha kwa kigezo cha ujumla kwamba ni Mkrelo, au pale anapokuwa amepewa mamlaka kisheria na Mamlaka yenye kuweza kutoa ruhusa hiyo yaani Askofu au Wakiri wa Askofu.[69]
Roho Mtakatifu yuko macho na anafanya kazi siku zote bila kupumzika, kwani yeye ni Roho wa Mungu. Roho huyo Mtakatifu hufanya kazi katika ulimwengu wote kwa kuwasaidia, kuimarisha, kufariji, kufundisha, kukumbusha, kubadilisha au kufanya watu wawe na uchaji wa Mungu kwa wote, wanaume na wanawake, wazee na vijana, watoto kwa wakubwa. Katika Sakramenti ya ubatizo tunampokea rasmi huyo “Roho Mtakatifu” na kwa tendo hilo tunajinyakulia hadhi ya kuitwa wana wa Mungu, kwani Mungu ametuzaa rasmi katika Ubatizo. Tena ni kwa Ubatizo tunapokelewa rasmi kuwa wanaushirika na Kanisa. Hivyo basi, kwamba Sakramenti ya Ubatizo ndio mlango pekee wa kuingia rasmi katika Ushirika na Kanisa la Mungu. Na hapo hapo, ni kwa njia ya Ubatizo Roho Mtakatifu anaingia kwa Muamini na kuanza kufariji kiroho na kifadhila (yaani, fadhila za Kikristu, Imani, Matumaini na Mapendo).

 5.3 SAKRAMENTI YA EKARISTI TAKATIFU

Ekaristi takatifu ni Yesu mzima, Mungu mtu chini ya umbo la mkate na divai. Ni sakramenti inayokamilisha hatua ya kumwingiza mtu katika ukristo. Ni chemchemi na kilele cha maisha yote ya Kikristo. Ukweli kwamba Ekaristi Takatifu ni Yesu mzima, Mungu-mtu chini ya umbo la mkate na divai haukubaliki kwa wengi, ingawa ukweli huu ni maneno ya Yesu Kristo mwenyewe. Yesu mwenyewe anasema; “Mimi ndimi mkate wa uzima ulioshuka kutoka mbinguni, aulaye mkate huu ataishi milele, na mkate nitakaotoa mimi ni mwili wangu kwa kuupatia ulimwengu uzima.”[70] Mtume Paulo pia anakiri uwepo wa mwili na damu ya Kristo katika maumbo ya mkate na divai baada ya mageuzo anaposema: “Kikombe tunachokibariki, je, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tunaoumega, je, si ushirika katika mwili wa Kristo? (1 Kor. 10:16).

5.3.1 Chanzo cha Sakramenti ya Ekaristi Takatifu

Sakramenti ya Ekaristi takatifu iliwekwa na Yesu Kristo mwenyewe, siku ya Alhamisi kuu pale alipokuwa akila karamu ya mwisho pamoja na wanafunzi wake. Katika hali isiyo ya kawaida siku hiyo Yesu alitwaa mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wafuasi wake akisema: “Twaeni mle wote; huu ndio mwili wangu, utakaotolewa kwa ajili yenu” Na baada ya kula alichukua kikombe chenye divai, akashukuru tena, akawapa wafuasi wake akisema; “Twaeni mnywe wote, hiki ni kikombe cha damu yangu, damu ya agano jipya na la milele itakayomwagika kwa ajili yenu na kwa ajili ya wengi kwa maondoleo ya dhambi; FANYENI HIVI KWA KUNIKUMBUKA MIMI.”[71]
Tumepokea masimulizi ya kuwekwa kwa sakramenti ya Ekaristi takatifu kutoka katika injili ndugu zote tatu na kutoka kwa mtume Paulo. Maandalizi ya kuwekwa kwa sakramenti hii tunayapata katika injili ya.[72] Tangu mwanzoni kanisa limebaki aminifu kwa amri ya Bwana: “Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume na katika ushirika na katika kuumega mkate na katika kusali…….. ilikuwa hasa siku ya dominika, siku ya ufufuko wa Yesu, wakristo walipokutanika kuumega mkate.”[73] Mt. Yustino shahidi mwaka 150 aliandika: “Tunachokipokea si mkate wa kawaida wala kinywaji cha kawaida; ila kwa vile Yesu Kristo mwokozi wetu alizaliwa  kwa neno la Mungu kwa ajili ya wokovu wetu, basi chakula kilichofanywa kwa sala ya Ekaristi iliyowekwa na Kristo mwenyewe ni kweli mwili na damu ya Kristo.”[74]
Mtaguso wa Trenti unatupatia ukweli ufuatao juu ya kuwekwa kwa Ekaristi: “Bwana, akishawapenda walio wake, aliwapenda upeo. Akijua kwamba saa yake ilishafika ya kutoka ulimwengu huu ili kurudi kwa Baba yake, walipokuwa wakila, aliwaosha miguu yao na aliwapa amri ya mapendo. Kusudi awaachie amana ya upendo huu, kusudi asijitenge kamwe na walio wake, na kusudi awafanye washiriki pasaka yake, aliiweka Ekaristi kama kumbukumbu ya kifo chake na ufufuko wake, na aliwaamuru mitume wake waiadhimishe mpaka atakaporudi, akiwafanya makuhani wa agano jipya.”[75]

 

 

5.3.2 Mhudumu wa Sakramenti ya Ekaristi Takatifu

Ni makuhani peke yao waliopewa sakramenti ya daraja takatifu kihalali wanaweza kusimamia Ekaristi na kugeuza mkate na divai kuwa mwili na damu ya Bwana. Makanisa mengine hawana Ekaristi takatifu kwa sababu hawana makuhani wenye Daraja Takatifu.[76]

5.3.3 Mwujiza wa mkate na divai kugeuka kuwa Mwili na Damu ya Yesu Kristu

Yesu Kristo aliyefanya muujiza wa kugeuza maji kuwa divai kule Kana (Yn 2: 1-11), Yesu aliyefanya muujiza wa kuwalisha watu elfu tano kwa mikate mitano (Yn 6: 1-12); ndiye pia anayefanya muujiza wa kugeuza mkate na divai kuwa mwili na damu yake kupitia mikono ya padre. Padre alipewa mamlaka haya na Yesu mwenyewe pale alipowaambia mitume: “Fanyeni hivi kwa kunikumbuka mimi”
Yesu alipochukua mkate na kusema huu ni mwili wangu, halafu baadaye akachukua divai na kusema hii ni damu yangu; wanafunzi wake waliendelea kuuona mkate na divai. Mkate na divai havikubadilika umbo la nje kuwa nyama na damu. Hata leo hii padre anapofanya muujiza huu; mkate na divai hugeuka kuwa mwili na damu ya Yesu kwa namna ipitayo ufahamu wetu ingawa maumbo ya mkate na divai huendelea kuonekana.
Wapo wengi ambao wanakwazwa sana na fundisho hili la Kristo, mbaya zaidi hata Wakatoliki wenyewe. Hali hii haitakiwi kutushangaza kwa sababu Yesu alipotoa tangazo la kwanza la Ekaristi takatifu wengi walikwazika na hata wanafunzi wake waligawanyika. “Neno hili ni gumu, ni nani awezaye kulisikia?” (Yn 6: 60).  Yesu anajua kwamba fundisho hili ni gumu, lakini hawezi kubadilisha ukweli kwa sababu watu hawaelewi. Ndiyo maana aliwaambia hata wanafunzi wake; “Je, ninyi nanyi mwataka kuondoka” (Yn 6: 67). Mkatoliki, swali hili ndilo ambalo Yesu anakuuliza leo: “Je, unataka kuondoka kwa sababu huelewi mkate na divai vinageukaje kuwa mwili na damu ya Kristo?”

5.3.4 Mambo ya kuzingatia ili kupokea vema Ekaristi Takatifu

1.  Lazima mtu awe mkristo mkatoliki ambaye yupo katika hali ya neema; maana yake asiwe katika dhambi ya mauti. “Kwa hiyo kila aulaye mkate au kukinywea kikombe cha  Bwana kwa hali mbaya anakufuru mwili na damu ya Bwana” (1 Kor 11: 27)
2.  Awe amesali sana na awe anamtamani Yesu. Ni wale tu wanaosali na kumtamani YESU wanaweza kujibu kama alivyojibu Petro Yesu alipouliza; “Ninyi nanyi mwataka kuondoka?” Petro alijibu: “Bwana, twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele” (Yn 6: 68)
3.  Pia awe ameacha chakula au kinywaji chenye ulevi muda wa saa moja. Maji anaweza kunywa wakati wowote. Mgonjwa anaruhusiwa kunywa dawa wakati wowote kabla ya kupokea. “Maana mwenye kula na kunywa bila kufanya tofauti kati ya mwili wa Kristo na chakula cha kawaida anajilia na kujinywea hukumu” (1Kor 11: 29)

5.3.5 Faida za Sakamenti ya Ekaristi Takatifu

ü Ekaristi hukuza muungano wetu na Kristo na Kanisa lake. “Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu hukaa ndani yangu nami hukaa ndanu yake” (Yn 6: 56).

ü Ekaristi Takatifu hutuondolea dhambi nyepesi na kupunguza hatari ya kutenda dhambi ya mauti. Huwezi kuungana na Kristo ukiwa katika hali ya dhambi; na hivi faida mojawapo ya ekaristi takatifu kutuosha na dhambi za zamani na kutukinga na dhambi zijazo. Muhimu ni kwamba,  Ekaristi takatifu haiondoi dhambi ya mauti. Ndiyo maana tunashauriwa kuungama kwanza kabla ya kupokea.

ü Ekaristi takatifu huilinda na kuongeza neema ya utakaso, tuliyopokea katika ubatizo na kipaimara iliyo uzima wa roho zetu.

ü Ekaristi Takatifu inadumisha na kustawisha mapendo ambayo katika maisha ya kila siku yanaelekea kudhoofika. Kwa mapendo haya ekaristi takatifu inaunda umoja wa kanisa. Ekaristi Takatifu inatufanya tuwe mwili mmoja katika Kristo.

ü Kwa Sakramenti ya Ekaristi Takatifu, tunatiwa nguvu na kuongezewa hamu ya kuurithi uzima wa milele. “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu anao uzima wa milele, nami nitamfufua siku ya mwisho” (Yn 6: 54)
Katika adhimisho la Ibada ya Misa Takatifu, wakati wa Mageuzo waadhimishaji, Padre au Askofu, humwomba Mungu amtume Roho Mtakatifu ili ageuze mkate kuwa mwili na Divai kuwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo.Si kwamba kabla ya Mageuzo hayo, Roho Mtakatifu anakuwa mbali, hapana. Ila tu, ni katika Mageuzo na kwa namna ya pekee Roho Mtakatifu anaombwa azishukie dhabihu hizo za Mkate na Divai lililo tunda la Mzabibu, ambalo halijachanganywa na chochote isipokuwa yale maji Padre anapochanganya mwenyewe altareni. Ili viwe Mwili na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo. Na kitendo hicho tunakiita sasa Epiklesis.
Epiklesis, Roho Mtakatifu anaombwa ashuke katika vipaji vya mkate na divai, kuzigeuza kuwa Mwili na Damu ya  Kristo. Kwa uwezo wake ubadilishao hufanya fumbo la Kristo litukie hapo linapoadhimishwa na katika wakati huo. Kuhani anaitandaza mikono yake juu ya vipaji kuonesha mpaji wa uzima Roho wa Mungu anamiminwa juu ya mkate na divai ili kuvigeuza kuwa Mwili na Damu ya Kristo. Wakoselebranti (Mapadre walioshiriki Adhimisho la Misa Takatifu) nao wanatandaza mikono yao kama kuhani kiongozi, isipokuwa kama wameshika kitabu hutandaza mkono mmoja.[77]
Roho Mtakatifu, Katika maadhimisho ya Sakramenti nyingine licha ya Upatanisho.Tukifahamu kuwa, Roho Mtakatifu ndiye Mtendaji Mkuu katika Maadhimisho ya Sakramenti zote.Kwa namna ya pekee anafanya kazi katika Adhimisho la Misa Takatifu inayoadhimishwa na kuhani (Padre, Askofu, Papa, Baba Mtakatifu naye ni Askofu wa Jimbo la Roma). Ni kwa nguvu ya Roho Mtakatifu dhabihu za Mkate na divai, zinageuka kuwa mwili na damu ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Padre anamsihi Mwenyezi Mungu amtume Roho Mtakatifu ili dhabihu za mkate na divai viweze kuwa mwili kabisa wa Yesu na danmu azizi ya Yesu, Ekaristi Takatifu, inapatikana katika Misa Takatifu. Na kuhani ndiye mwenye ofisi hiyo ya kuadhimisha fumbo zima la Ekaristi Takatifu, akijifahamu kuwa yeye ni chombo kinachotumika kuwaunganisha Waamini na Mungu kwa tendo la adhimisho la Misa Takatifu.
Katika adhimisho la Misa Takatifu, wakati wa Mageuzo, Padre anamwomba Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu mkuu Roho Mtakatifu aweze kubadili maumbo ya mkate na divai viweze kugeuka kuwa Mwili na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, anasema “Basi ee Bwana tunakusihi umtume Roho wako Mtakatifu dhabihu hizi umtume Roho wako Mtakatifu aweze kugeuza mkate na divai viwe mwili na damu ya Bwana wetu Kristu ’’. 
Roho Mtakatifu anatia mioyoni mwa Familia ya Mungu juhudi ya kutangaza Injili.Yeye ndiye mwinjilishaji mkuu katika harakati zetu za kuinjilisha ulimwengu.Ni pamoja na kuhimiza Sala katika familia na katika jumuia ndogo ndogo za Kikristo. Roho Mtakatifu kwa sala zetu tukimwomba, Ulimwengu hutakatifuzwa, Baba Mtakatifu, Maaskofu, Mapadri, Watawa wa Kike na Wakiume, Wanafamilia na Vijana wetu. Roho Mtakatifu hutakasa huwanyunyizia makundi mbalimbali ya Vyama vya Kitume wakijiweka katika Sala na usikivu wa NENO la Mungu (Maandiko Matakatifu ya Biblia). Roho Mtakatifu huwezesha kupata kila aina ya Neema na Baraka wanazohitaji katika maisha yao.
 Kwa upande wa wale wanaopokea Sakramenti ya Ekaristi Takatifu waliobatizwa utotoni wanapaswa watayarishwe na wapewe sakramenti ya Ekaristi Takatifu wakiwa wana jua vema ukuu wa Sakramenti hii. Kwamba kweli wanampokea Yesu Kristo mzima katika maumbo ya Mkate na divai. Na baada ya Komonio ni vema yawepo mafundisho endelevu hadi watakapofuata mafundisho ya Kipaimara.
Baada ya mageuzo, mkate na divai vinakuwa kweli mwili na damu ya Yesu, na katika kila kipande cha HOSTIA mnakuwa na Yesu kristo mzima, Mungu-mtu. Mkate na divai hugeuka kuwa mwili na damu ya Yesu hata kama padre anayefanya mageuzo hayo ana dhambi ya mauti kwa sababu anayefanya mageuzo ni Yesu mwenyewe.
Kwa kuwa Kristo mwenyewe yumo katika sakramenti ya Ekaristi takatifu ni lazima kumheshimu kwa ibada ya kuabudu. Na hivi ni wajibu wa wakristo kuabudu sakramenti kuu hii kwani hicho ndicho kipimo cha shukrani na ishara ya mapendo yetu kwa mkombozi wetu.

5.4 SAKRAMENTI YA NDOA

“Yapo makosa mengi sana duniani, ukikosea wa kuoa au wakuolewa naye. Hilo ni pigo katika Maisha yako yote. Na kila mwanajamii atakaye kuona ukiwa na simanzi za fujo katika ndoa yenu atatikisa kichwa kwa kukusikitikia. (Inatoka kwenye Misemo ya Hekima kwa kabila ''Wasukuma'') Na hakuna mtu mwenye mapenzi mema katika jamii angefurahia kuona wanandoa majirani wanaishi kwa kukimbizana na kuishi maisha ya vurugu siku zote.’’ Kumbe ni vema wachumba wachunguzane kwa kipindi kirefu kuhusu tabia zao na na sio uchumba unaofanywa baada ya kukutana kwenye basi au ‘’treni ‘’(gari moshi) au kwenye kituo cha mabasi.
Ni busara ya Kanisa Katoliki kuzidi kusisitiza siku zote mpaka leo kuwa wakatoliki wanapotaka kuweka uchumba; wasali sana, ili Mungu awasaidie kupata wachumba wema. Kanisa linaongezea kutoa ushauri kwa wanaotaka kuoa; Waulize shauri kwa wakubwa wao, kama tunavyotafakarishwa na neno la Mungu kwa maonyo, likisema:  ‘Mwanangu usifanye kitu bila shauri; hivyo hutakuwa na kujuta baada ya kufanya.’[78]
Kwa ustawi na uimara wa ndoa, Kanisa Katoliki linamuasa mkatoliki anapotaka kuoa au kuolewa achague mchumba aliye pia mkatoliki au atakayekuwa mkatoliki baadaye. Wakati wa uchumba wa uchumba watunze usafi wa moyo, wapokee Sakramenti za Kitubio na Ekaristi takatifu mara nyingi. Sakramenti ya ndoa yawalazimu watu wa ndoa:  kuishi uimara wa ndoa yaani kukaa pamoja kwa uaminifu mpaka kufa, kupendana na kusaidiana, kupenda kupata watoto, kuwalea vyema na kuwaongoza kwa Mungu.
Hivyo basi ,ndoa haiwezi kufunguliwa wala na Kanisa wala na Serikali  ila kwa kufa tu, kwani  ndoa  Katoliki ni Sakramenti na hivyo basi, ndoa naiheshimiwe.Madhara ya ‘’mparanganyiko’’ wa wanandoa kisaikolojia huwaathiri mpaka watoto na hata wajukuu pia.

5.4.1 Asili ya Ndoa

Mungu mwenyewe ndiye asili ya Ndoa . Hivyo basi ndoa yatoka kwa Mungu.Kama ndoa   inatoka kwa Mungu. Kwanini sasa isiheshimiwe? Katika maandiko Matakatifu tunasoma, Kisha Mwenyezi Mungu akasema, “Si vizuri huyu mwanamume kuwa peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa (Rej. Mw 2:18). Na tunasoma tena kuwa ni kutokana na ubavu wa mwanamume hapo mwanamke alipatikana baada ya Mungu kumpa Mwanaume usingizi mzito tunasoma “Basi, Mwenyezi Mungu akamletea huyo mwanamume usingizi mzito na alipokuwa usingizini, akamtwaa ubavu wake mmoja na kupafunika mahali pale kwa nyama. Na huo ubavu Mwenyezi Mungu alioutoa kwa yule mwanamume akaufanya kuwa mwanamke akamleta kwa huyo mwanamume. Ndipo huyo mwanamume akasema “Naam ! Huyu ni mfupa kutoka mifupa yangu na nyama kutoka nyama yangu. “Huyu ataitwa “Mwanamke’’ kwa sababu ametolewa katika Mwanamume’’. Ndiyo maana mwanamume humwacha Baba yake na Mama yake, akaambatana na mkewe, nao wawili huwa mwili mmoja (Rej. Mw 2:21-24).
Mungu anaupinga “Ulimbukeni”  wa watu wanaojiita wanakwenda na wakati ‘’ Kila mtu atakaye mwacha mkewe isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine azini, naye amwoaye yule aliyeachwa azini (Rej. Mt 19:9). Sababu iliyotolewa na Yesu ya kuachana kwa sababu ya Uasherati iliongelewa katika mazingira ya mwandishi alimaanisha kuwa kwa wale wanaooana huku ni ndugu wa damu mfano, Kaka na dada au Baba na bintiye hata kama walifunga ndoa Kanisani kwa kujificha au kumdanganya Padre au Shemas, hapa tunaiita ni “batili’’ kumbe sasa hata haikuwa ndoa kwani hakuna ndoa baina ya ndugu wa damu.[79] Kumbe basi, ndugu wa damu iwe kwa uhusiano wa kisheria au wa kiasili wanazuiwa na Kanisa kufunga ndoa.Na hiyo kwa kweli ni Sheria ya Mungu na hakuna mamlaka yoyote chini ya jua yanayoweza kuipindua wala kuibadilisha.
Na matokeo yake wanajikuta wamo katika maisha ya kuishi kwa mikataba na baadaye wanabaki mitaani wana wayawaya bila kuwa na mbele wala nyuma. Na watoto “wanapigika’’ kwa kukosa malezi ya wazazi wao.

5.5 SAKRAMENTI YA KITUBIO


Wakati mwingine inaitwa Sakramenti ya Huruma ya Mungu au ya Kujipatanisha na Mungu. Na hivyo Roho Mtakatifu ndiye huzikumbusha na kuzisuta dhamiri zetu pale tunapokuwa tumemkosea Mungu, pale tunapovunja amri zake Mwenyezi Mungu. Ni Roho Mtakatifu anayetupatia mguso na msukumo wa kwenda kwenye Sakramenti ya Upatanisho (Maungamo na Toba ya kweli).
Tujongee kwenye kiti cha Huruma (Kwenye Maungamo) bila woga wowote ili tutakaswe, na kuondolewa dhambi zetu.Kwani dhambi ni adui wa Roho wa Mungu. Tunapotenda dhambi tunamfukuza Roho Mtakatifu, Kwani Miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu kama Mtume Paulo anavyosema. Pia kwa kujisomea unaweza kufunua Biblia Takatifu Tuishi tukiongozwa na Maisha ya Roho wa Mungu  (Gal 5:25 , 2:17,3:13 ;  1Kor 15:45; Rum 8:2)
Tumkimbilie Kristo, kwa kupitia Mtumishi wake Padre, aliyekuhani na Kristo Mwingine atuondolee dhambi zetu, pale tunapojikuta tumekurupusha amri za Mungu. Kwa daraja ya Upadre, Padre anapewa mamlaka ya kuondolea dhambi kwa wale wanaomkimbilia ili wajipatie rehema na utakatifu kwa Mungu. Kujitakasa kiroho kwa Sakramenti. Tuzingatie sana kuishi tukiwa na Roho safi na dhamiri zisizokuwa na “makunyanzi.’’
Sakramenti ya Kitubio au Upatanisho ni muhimu sana katika maisha yetu. Yesu mfufuka aliwaambia mitume wake “Amani kwenu’’ kama vile Baba alivyonituma mimi nami nawatuma ninyi. Alipokwisha sema hayo; Akawavuvia na Kuwaambia ‘’ Pokeeni Roho Mtakatifu; Mkiwaondolea watu dhambi zao wataondolewa, msipowaondolea, hawataondolewa.[80] Hiyo ni moja ya kazi muhimu sana za Roho Mtakatifu katika Kanisa. Na Mkatoliki yeyote yule anayedharau Sakramenti Takatifu yoyote, ajue yuko mbioni kutengwa na kanisa au ameshajitenga yeye mwenyewe moja kwa moja kwa kujua au kutojua.Angalisho kwa vyama vya Kitume na Vikundi vya Sala tuwe macho, tuheshimu Sakramenti zote Saba. Baada ya kuona kuwa Sakramenti ya Kitubio haipokelewi na wengi kuna haja kubwa sana iwepo  nia na mpango  madhubuti wa kuifanya sakramenti hii ipendwe na waamini wapewe upya  Katekesi,  na waone umuhimu wake katika maisha.

5.6 SAKRAMENTI YA MPAKO WA WAGONJWA


Mpako wa wagonjwa ni sakramenti inayomtia nguvu Mkristo aweze kuyapokea maumivu na shida katika magonjwa yake akimtumainia Yesu Kristo aliye Mwokozi wetu.Sakramenti ya mpako wa wagonjwa huweza kumponya Mkristo Kiroho zaidi na kimwili pia.
Ni kwa Sakramenti ya mpako wa Wagonjwa na Sala za Makuhani, kanisa  lote huwakabidhi wagonjwa kwa Bwana  aliyeteswa na kutukuzwa ili awainue na kuwaokoa. Na kwa hakika lawahimiza wajiunge kwa hiari na Mateso na Kifo cha Kristo ili kutoa mchango wao kwa manufaa ya Taifa la Mungu.[81] Ni Mungu katika Utatu Mtakatifu mwenye kumponya mgonjwa kiroho na kimwili. Roho Mtakatifu humpatia ujasiri mgonjwa aweze kuyapokea maumivu kwa imani katika kumtegemea Mungu mwenyewe aliye asili ya afya na uhai wetu kwa ujumla. Yesu Kristo aliyepata mateso makali msalabani haachi kumfariji mgonjwa.Pia Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa ni ishara ya matumaini, kumwachia Mungu aweze kutenda kadiri ya Mapenzi yake. Mkristo anaalikwa na Mama Kanisa kuwa na imani, kusadiki. Kristo mwenyewe aliwataka wagonjwa wasadiki kwamba nguvu ya Mungu inatenda kazi. Kristo ni Mganga aliweza kutumia ishara mbalimbali katika kuponya wagonjwa kama vile mate na kuwekea mikono, tope na kuosha.
Ndio maana tunaambiwa  kuwa Yesu Kristo  alipokuwa kwenye utume wagonjwa walimtafuta angalau wamshike hata upindo wa vazi lake. Tunasoma pia, kwa nguvu ya ufufuko wa Yesu Kristo, wagonjwa njiani walitamani hata kivuri cha mtume Petro kiwafikie tu wapate kupona. Waliamini kuwa wangeponywa na Mtume Petro, kwani alikuwa ameshafufua mfu. Hivyo hivyo ni katika Sakramenti ya Mpako wa Wagonjwa Kristo anaendelea kutugusa. Ni wajibu wa Wakristo wote kuwapoza wagonjwa, kuwafariji, kuwasaidia kwa hali na mali.

5.7  SAKRAMENTI  YA DARAJA TAKATIFU


Ninaposema Daraja Takatifu (Holy Orders), nina maana ya yale Madaraja matatu; yaani Daraja ya Ushemas, Daraja ya Upadre na Daraja ya Uaskofu. Kwa namna nyingine Daraja ya Ushemas inaitwa Daraja ya tatu ya Ukasisi. Pia Daraja ya Upadre inaitwa Daraja ya pili ya Ukasisi. Na Daraja ya Uaskofu inaitwa Daraja ya kwanza ya Ukasisi. Daraja hii ya kwanza ya Ukasisi ndiyo inayompa Askofu kuwa na ule uwezo na nguvu kuu ya Upadre (A Bishop has that fullness of Priesthood) tofauti na madaraja mengine mawili ya Ushemas na Upadre. Kwani Askofu ndiye Jimbo na ndiye mwenye mamlaka yote katika Jimbo husika. Mashemas na Mapdre hawa ni wandamizi wa Askofu, wapo kumwakilisha na kumsaidia kazi za kitume popote pale anapotamani kuwepo; lakini anakuwepo kwa uwakilishi wa watu hao.
Historia ya Daraja Takatifu na uhtaji wake
Katika Kanuni ya Imani, tunakutana na sehemu inayosema “Roho Mtakatifu aliyenena kwa vinywa vya Manabii’’ ni ushahidi tosha kabisa na hatuna shaka, hii ndiyo ungamo la Imani la Kanisa Katoliki. Roho Mtakatifu alitenda kazi ndani ya Manabii katika Historia nzima ya Wokovu wa mwanadamu. Katika Agano la Kale tunakutana na uvuvio wa Roho Mtakatifu kwa Manabii na hilo tunaliona kuanzia Nabii Musa.
“Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Waisraeli na atasamehewa kwa sababu  si kosa walilokusudia na wameleta sadaka yao ya kuteketeza kwa Mwenyezi Mungu  kama dhabihu na sadaka ya kuondoa dhambi kwa ajili ya kosa lao.’’[82]
Pia, “Naye Mose akamwomba Mwenyezi Mungu, Ee Mwenyezi Mungu, Mungu uliye asili ya Uhai wote, nakuomba umteue mtu wa kusimamia   jumuiya hii, Ambaye atawatangulia na kuwaongoza katika shughuli zao zote, ili wasije wakawa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji.”[83]
Tunaona jinsi Nabii Mose alivyomwomba Mwenyezi Mungu  amteue mtu wa kuwaongoza taifa la  Waana wa Israeli naye ni Yoshua mwana wa Nuni, tunaambiwa Yoshua alikuwa mtu mwenye  Roho nzuri,aliyepaswa kuwekewa mikono na asimamishwe mbele ya Kuhani Eleazari.Tunazidi kuambiwa  kuwa kuhani Eleazari alimwekea mikono kichwani Yoshua na kumpa mamlaka kama alivyoagizwa na Mwenyezi Mungu.[84]
Ishara ya Kuhani Eleazari ya kumwekea mkono juu kichwani mwa Yoshua inamaanisha kumwomba Roho Mtakatifu amshukie Yoshua aweze kufanikisha vema na salama kazi ya Mungu ya kuwaongoza Waisraeli katika safari ya kuelekea nchi ya ahadi. Madhehebu haya ya kuwawekea Mikono kichwani yamebaki katika Liturujia ya kuwaweka wakfu Makuhani wa Mungu, yaani katika adhimisho la Misa ya kumweka wakfu Shemas, Padre na Askofu. Kwa kumwekea mikono ni kumwomba Roho Mtakatifu aweze kumshushia mapaji yake katika huduma ya Ushemasi, Upadre au Uaskofu. Roho Mtakatifu anamwongoza “Mtoa huduma wa Mungu” (Kuhani) aweze kulihudumia kanisa kulingana na Matakwa ya Mwenyezi Mungu kama vile Yoshua alivyopaswa kulitumikia vema taifa teule la Mungu (Waisraeli).
Basi Roho ya Mwenyezi Mungu ikamjia Othnieli, naye akawa mwamuzi wa Waisraeli. Roho wa Mungu alikuwa naye. Othniel alikuwa ni jibu la ombi la Waisraeli baada ya Mungu kuuficha uso wake mbele ya Waisraeli kwani Waisraeli walikengeuka na kuirudia miungu ya uongo mabaali na maashira.[85] Waisraeli walitenda uovu mbele ya Mwenyezi Mungu wakamsahau Mwenyezi Mungu, Mungu wao,wakaabudu Mabaali na Maashera (miungu ya kipagani).
Basi hasira ya Mwenyezi Mungu ikawaka dhidi ya Israeli … Hata hivyo  agano la Kale bado linaonesha nguvu ya Roho Mtakatifu, Kitabu cha Kwanza cha Samweli (1Sam 10:6) ,ambapo tunasoma ‘’Roho  ya Mwenyezi – Mungu itakujia kwa nguvu ,nawe utaanza kutabiri pamoja nao na kugeuka kuwa mtu mwingine, Hapa Samweli anaendelea kupata mahusia na maneno yenye kumpatia nguvu katika kutekeleza yale Bwana Mungu aliyomwamuru, katika Mstari wa Sura hiyo ya 10,  Samweli  anaelezwa kuwa  Wakati mambo hayo yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya kifanye, kwani Mungu yu pamoja nawe.  Ama kweli haya ni maneno ya Faraja na yenye kutia nguvu kwa Mhudumu wa kazi zimuhusuyo Mungu.
Ni neno lenye kuonesha tumaini na Moyo Mkuu ambamo Roho Mtakatikifu aliye Mungu hutoa paji lake la Faraja. Roho huyu Mtakatifu mwezeshaji wa shughuri zote za Kumuhubiri Yesu Kristu. Kazi za Roho Mtakatifu zinajifunua katika kuonesha nguvu ya KiMungu katika maisha ya mwanadamu.


SURA YA SITA

UKIIPENDA DUNIA, KUMPENDA MUNGU HAKUKO NDANI YAKO

6.0 UTANGULIZI


 “Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda Yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto, kwa sababu mmemjua Baba. Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.  Msiipende  dunia, wala  mambo  yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. Maana kila kilichomo duniani, yaani, tama ya mwili, na tama ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia”[86]   Lakini vilevile maisha yetu yananena juu yetu kuwa, “ hao ni wa dunia; kwa hiyo wanena ya ya dunia na dunia huwasikia.”[87]
Naomba tutafakari namna mbili tu ambazo ni miongoni mwa milango ya fahamu mitano (5) ya mwanadamu. Nayo ni Sikio na Macho, ambazo zinafanya kazi kwa ukaribu sana. Hivyo ni milango ya fahamu inayotegemeana kwa lugha nyingine. Upofu unakuondoa kwa vitu lakini kuwa kiziwi kunakuondoa kwa watu. Hausikii ushauri wao, nasaha zao, onyo, maneno ya kutia moyo na pongezi. Usipoweza kusikia utasahau na namna ya kuongea. Padre wa Kanisa Katoliki anapombatiza mtoto mdogo anamgusa mtoto masikio na kinywa kwa kidole gumba akisema, “Bwana Yesu, aliyewafanya viziwi wasikie, na bubu waseme, akujalie uweze kusikia kwa masikio neno lake, na kuungama kwa mdomo imani ya kikristu, kwa sifa na utukufu wa Mungu Baba”

6.1 Namna ya Jicho au Macho


Wapendwa ndugu zangu katika Kristu, vijana na walezi na kwa namna ya pekee wewe msomaji au wasomaji wa kitabu hiki. Napenda nitafakari nanyi juu ya jicho, tukiongozwa na masomo ya Maandiko Matakatifu; Yoshua Bin Sira 17:1,6-14 na Matayo 6:22-23. Jicho ni mojawapo ya njia za fahamu zilizo kwenye kichwa. Kichwa ni sehemu yenye viungo kama ubongo, wenye kazi nyingi kama vile kufikiri, njia za fahamu kama vile jicho, mdomo, masikio, pua na sehemu ndogo ya ngozi. Haya yote yameumbwa na Mungu na ni zawadi kama tulivyosikia kwenye somo la kwanza. Katika kutenda kwake jicho na sehemu nyingine za mwili husika- husaidiana. Kichwa ni injini ya mwili. Mt. Lucia anatufundisha akisema “jicho ni moyo wa nje wa mwili wetu linaloonyesha maisha ya ndani ya kila mmoja wetu. Limefanywa kwa  ajili ya mwanga ili liweze kuona, kutafakari na kumpenda Mungu na viumbe katika ukweli na upendo, katika uzuri na usafi wa moyo, katika haki na utakatifu. Tulilinde na maovu yote ya kiroho na kimwili.”

6.1.1 Kazi ya Jicho au Macho

Ø Jicho ni moyo wa nje wa mwili wetu; moyo ulioko ndani ya mtu hufanya kazi ya kusukuma damu, ni pampu ya damu. Jicho kama moyo wa nje, hutusukuma kutenda tuyaonayo. Moyo hutamani kutenda, kumiliki na kutawala. Jicho pia kama moyo wa nje wa mwili husukuma mwili kutamani na kutenda. Jicho likiona kitu kizuri mfano gari zuri, nyumba nzuri au binti mzuri au picha yake nzuri kwenye mtandao au studio, tembea yake na mitikiso ya mwili, mwili mzima unapagawa, unahemka au binti akiona mvulana mzuri, mwili wake mzima unasisimka, unatamani. Siku hizi tamaa ziko nyingi mno, tamaa ni maisha ya ndani ya mtu-kiumbe.
Ø Jicho linaonyesha maisha ya ndani ya kila mmoja. Jicho huonyesha wema, uzuri, uso wa kimalaika wa mtu pamoja na ubaya, udanganyifu, ufisadi, wivu, kashfa, kiburi, upumbavu Mk. 7:21, Mt. Paulo naongezea katika waraka wake kwa Wagalatia 5:19, kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, mabishano, mafarakano, hususda, ulevi, ulafi, kijicho; haya yote ni matendo ya giza lakini…
Ø Jicho limefanywa kwa ajili ya mwanga. Yesu aliwaambia Mafarisayo, jicho ni taa ya mwili (Mt. 6:22-23). Basi, kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga. Lakini, ikiwa jicho ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga  uliona ndani yako ni giza, basi hilo ni giza,, na hilo ni giza la kutosha mno. Giza huwa linapotosha (povusha).
Ø Jicho limefanywa ili kuona. Kama vile tulivyotaja hapo juu vipo ndani yako basi kwako mwanga ni giza ni giza na kama kwako mwanga ni giza, basi giza ulilonalo ni giza hasa. Ni giza kweli kweli, ni giza topea, pitahulka. Moyo huo wa nje wa mwili wetu umekufa. Jicho halioni. Linafunguka mpaka mwisho lakini halioni. Nabii yuko sahihi wana macho lakini hawaoni. Mt. Yohane anatueleza maisha halisi, juu ya giza, wale waliokaa katika giza la uvuli wa mauti, matendo ya giza tumeyataja juu.
Ø Jicho limefanywa ili kutafakari. Sasa wangapi tuna tumia macho yetu kupitisha vitu safi vya kutafakari? Kwenye mtandao mnachukua vitu gani? Jicho linapendelea kuangalia nini na kusoma nini? Jicho limefanywa kwa ajili ya uzuri na usafi wa moyo (Mt. Lucia ansema). Asilmia 75 ya habari na elimu tuliyonayo hutokana na kuona kwa jicho. Kwa jicho tunaona na baadae tunatafakari hekima na upumbafu, maarifa na ujinga, uzuri na ubaya, Mungu na shetani, ya mwili na kiroho. Lakini jicho limefanywa ili tumtafakari Mungu na si ubatili.
Ø Jicho limefanya ili kumpenda Mungu. Hivyo mambo ya kiroho, kimbingu na kimungu, hekima ya matendo ya watu, hayo yote ndiyo yanayotupatia  heshima, uadilifu na utakatifu. Na si mambo ya mwili, kidunia na ya binafsi wa ubinadamu wetu.
Ø Jicho limefanywa ili kuvipenda viumbe. Kama vile anga, nyota, sayari, mwezi, jua, bahari, milima, mabonde, mito, miti, wanyama, wadudu, ndege, vifaa vya sayansi, matokeo ya teknolojia, haya yote ni kweli za maisha. Kutokana na maajabu haya tuzidi kumpenda Mungu, na si kuviharibu. Askari anaweza kupofukia vitani lakini wanaokwendahuko wana macho wote, wanaharibu kila kitu… jicho limefanywa kwa ajili ya ukweli na upendo, haki na utakatifu (Mt. Lucia) ili kwa akili na njia zote za fahamu zilizo kichwani (mdomo, pua, ngozi na masikio, tungekuwa na muda tungetafakari haya) tuweze kuwa watu wa ukweli na upendo, haki na utakatifu.
Imani ni jicho la roho. Basi tunzeni macho yenu, mboni za macho yenu, kwa kuwa jicho ni kwa ajili ya Mungu. Na Mt. Lucia anatundisha “tulilinde jicho na maovu yote ya kiroho na kimwili.”

 



6.2 Jifunze kitu juu ya Sikio


Kwa kutambua na kujua namna sikio linavyoweza kupata kitu kupitia sauti, kunahusianishwa zaidi na Akili ambapo baada ya pinna kukusanya yale mawimbi ya sauti kutoka kila kona ya dunia ndipo hapo mawimbi hayo yanatumwa kwenye ubongo kwa ajili ya kutolewa ripoti ya taarifa ambayo hutujia na kutuelewesha nini kilikuwa kikiongelewa. Kwa kuwa yeye aliyetuumba ni mweza vivyohivyo ukijaribu kutafakari juu ya mchakato unavyofanyika mpata ujumbe kutumwa inafanyika haraka sana kwa uwezo aliotukirimia huyu mwumba wetu. Mafundisho haya ni yamejikita katika mlalo kulingana na kile alichotoa Fr. Faustin Kamugisha tarehe 7/09/2012, pamoja na mengine mengi kulingana na uzoefu wangu.  
Kiziwi hafokewi. Ni msemo wa kiafrika. Mtu aliye na matatizo ya kusikia hatakuelewa ukimfokea. Tukumbuke kuwa licha ya sikio la kimwili kuna masikio ya kiroho au ya moyo. Ni katika msingi wa masikio ya moyo tunasema, asiyesikia la mkuu huvunjika guu. Si suala la kusikia la masikio ya kimwili bali kusikiliza na kuzingatia na kuyafanyia kazi. Kuna mwanaume aliyekuwa anasoma gazeti akumuomba amusomee mke wake utafiti uliofanywa. Mwanaume akasoma, “Utafiti umegundua kuwa wanawake wanaongea maneno mengi mara mbili ya wanaume.” Aliposema hivyo mke wake asema, “ Tunasema meneno mengi kwa vile tukisema mara ya kwanza hamsikii.” Hapo mme wake akauliza, “Hivi unasemaje?” Mwanamme huyo alifokewa na mke wake. Ni katika msingi huu tunasema, kiziwi hafokewi. Kumfokea mtu huyu hakutamsaidia.
Kwa kurejea Mithali 20:12 anatujuza “Sikio lisikialo na jicho lionalo, Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili”. Hivyo kwa utambuzi huo kwamba limeumbwa na Mungu mwenyewe akiwa na nia nzuri kabisa kwetu sisi, hatunabudi kulitumia vema kama alivyonuia tulitumie yaani katika matumizi sahihi kabisa. Na kama tusipofanya hivyo basi tunakuwa tunakiuka maadili na hivyo kutufanya au kutupelekea katika kutenda dhambi. Ndipo hapo linatimia lile neno la wahenga lisemalo “Sikio la kufa halisikii dawa.” Nasi vivyohivyo kama tutakaa na kusikiliza kila jambo linalonenwa pengine juu yetu, tutakuwa tunauendekeza upagani, ambapo tutaanza kuwa watu wa chuki, fitina, na wazuri wakusengenya wenzetu yaani kwa kuwa mashushushutu.
Kwa kuwa tunajua na kutambua mwili ni mmoja tu ,bali una viungo vingi na kila kimoja na kazi yake binafsi. Vivyohivyo kama ilivyo kichwa kimoja ila kina viungo mbalimbali na vilivyotofautitofauti kama vile Sikio=kusikia au kusikiliza, Jicho=kuona, Pua=kunusa, Ulimi=kulamba na Ngozi =kuhisi. Lakini sikio linahusiana sana na mdomo ambao injini yake ni ulimi katika kutenda na kufanyakazi ya mawasiliano kwa vitendo.
Tukirejea Wagalatia 5:19-21 tunaona matendo yaliyo ya kimwili ambayo yanasababishwa zaidi na viungo vyetu vya mwili kama yalivyotajwa katika andiko hilo. Kwa mfano, ugomvi, fitina au uzushi, hasira ambavyo tunavipa nafasi kubwa ya kutenda na kufanyika kupitia sikio baada ya kusikia. Hapo jibu lake siku zote linajibiwa kwa uharaka na mdomo kupitia ulimi bila kusita, na hivyo kutufanya sisi kugeuka kuwa kama wanyama wengine kupitia matendo yetu yanavyo kuwa yakienenda kama shetani, maana kama tunaweza kusikia na mara moja tukakifanyia kazi bila kufikiri mara mbili wakati tumepewa utashi wa kung’amua lipi jema na lipi baya. Na kama Yoshua Bini Sira 18:19 anatuasa kuwa tujifunze kabla ya kunena, na siyo kila tulisikialo linatupasa kulitolea majibu kwa kunena laa! hasha, keti utafakari.
Kupitia tuyasikiayo, mdomo umekuwa kimbelembele kunena tu, na mwisho kujaza chuki baina yetu. Kikubwa basi lazima tufike mahali tuifunge au kuituliza midomo yetu. Hapo kama ilivyo “si kila avumaye baharini ni papa laa! Hasha ana wengine wamo”. Vivyohivyo si kila tulisikialo tuliamini na kulipa nafasi au uzito kwa asilimia zote 100%, ndiyo maana hata kiwango cha mashine kufanyakazi hakifikii 100%. Tukirejea YBS 33:19 anatuasa kusikiliza na kutegea masikio yetu kwa makini ili tuelewe na kuweza kuchanganua maneno hayo au maana ya sauti hizo.
Mk. 7: 33-37 juu ya EFATHA  Na mwisho kabisa ndiyo maana hata katika ubatizo wa watu kwenye kipengele cha EFETA kwa kuanza na maneno yafuatayo ”BwanaYesu, aliyewafanya viziwi wasikie, na Bubu waseme akujalie uweze kusikia kwa masikio neno lake, nakuungama kwa mdomo imani ya kikristu, kwa sifa na utukufu wa Mungu Baba. Amina. Tunaambiwa kwa kutajwa jina Mfano  Flavian EFETA sikia, funguka. Yaani Padre anafanya Ishara ya msalaba katika sikio na kumalizia kwenye mdomo, ikimaanisha kwa kile tukisikiacho tukapate kukinena kwa midomo yetu ilimradi kiwe cha kumtukuza Mungu.  Kwahiyo ndugu zangu tujitahidi kuitumia midomo yetu vema, pia kuwa makini kwa sauti zote tusikiazo ili kabla ya kuamua chochote tukifikirie mara mbili kwa kuangalia pande zote za shilingi yaani Upande wa faida na hasara.
kuna kutia vidole masikioni.[88] Alimgusa. Mara masikio yake yakafunguka.....(rej. Mk 7:35) Ambaye hasikii mguse kwa neno alopendelea kwanza. Mtu hasikilizi ujumbe sababu ujumbe haujamgusa. Mguse kwa mambo ambayo kwake ni kama ngozi yake. Ni sehemu yake. Kwa mfugaji Yesu ni mchungaji. Ni malisho. Kupitia hapo mfugaji ataanza kukusikiliza. Kwa hakimu na jaji Yesu ni mshauri wa ajabu. Kwa fundi seremala Yesu ni mlango. Ni katika msingi huo ili wenye shida ya maji wakusikilize lazima uwaguse kwa kuongelea shida ya maji na kutafuta uvumbuzi. Ujumbe kuhusu watoto au mwanaume utamfanya mwanamke aanze kusikiliza.

6.2.1 Mfano wa Yesu na Kiziwi

“Wakamletea kiziwi, naye ni mwenye utasi wakamsihi amwekee mikono. Akamtenga na mkutano faraghani, akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate, akamgusa ulimi akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia Efatha, maana yake, funguka. Mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri”  (Marko 7:32-35). Kuna matendo saba katika kumtibu kiziwi na bubu. (1) Akamtenga na watu (2) Akatia vidole vyake masikioni (3) Akatema mate (4) Akamgusa ulimi (5) akatazama juu mbinguni (6) Akaugua (7) akamwambia Efatha. Kwanza  ni kutengwa na watu. Watu wanaweza kumfanya mtu asisikilize. Kuna saikolojia ya umati au mkutano inaitwa kwa Kiingereza “mob psychology.” Wakati mwingine maneno anayopata mwanamke toka saluni yanaweza kumfanya asimsikilize mume wake. Maneno anayopata mwanaume toka kilabuni yanaweza kumfanya asimsikilize mke wake. Lazima tuachane na marafiki wabaya wenye ushauru mbaya.
Tatu akatema mate. Mate ni ya kulainisha. Ambaye hasikilizi anahitaji jambo la kumlainisha. Linaweza kuwa neno zuri au neno la kutia matumaini, au kumsikiliza kwa makini akiongea. Kumsikiliza mtu kwa makini ni kumlainisha. Lenin aliweza kusikiliza kwa makini kiasi cha kumchokesha mzungumzaji. Usiseme fulani hanisikilizi nawe msikilize.
Nne ni kumgusa mtu ulimi. Mpe mtu ambaye anafanya makosa kwa kutumia ulimi utaratibu wa kutumia ulimi. Mwenye kuongea sana akajikuta hasikilizi wengine anahitaji ukimya. Kuna watu ambao wanaposikia pointi moja wanafikiria namna ya kujibu pointi hiyo na hawatilii maanani poinyi nyingine. Wanahitaji utamaduni wa kuwa kimya. Baba mmoja wa busara wa Kijapani, wakati wa kipindi cha Meji  (1868-1912) alipokea mgeni aliyekuja kuuliza juu ya siri ya mafanikio. Lakini badala ya kusikiliza, mgeni huyo aliendelea kuongelea mawazo yake. Kitambo kidogo baadaye, baba mwenye busara alimwandalia chai. Aliweka chai kwenye kikombe cha mgeni mpaka kilipojaa pomoni ,aliendelea kujaza chai bila kukoma. Hatimaye mgeni hakuweza kujizuia, “Hauoni kuwa kikombe kimejaa?” alisema. “Hauwezi ukaongeza chai.”  “Namna hiyo hiyo, na kama kikombe hiki umejaa mawazo yako namna gani naweza kukuelezea siri ya mafanikio.” Sikiliza vinginevyo ulimi wako utakufanya uwe kiziwi. Ni methali ya Amerika.
Tano, Yesu alitazama juu mbinguni. Alitaka Mungu baba aingilie kati. Tunaambiwa na nabii Isaya,   “…Mungu atakuja na kuwaokoa ninyi. Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa…” (Isaya 35: 4-7). Tunahitaji msaada wa Mungu pengine kutambue kuwa sauti ya Mungu ni sauti ya watu. Tusikilize sauti ya Mungu. Kusikiliza sauti ya Mungu. Atupashwi kumwambia Mungu, “sikiliza mtumishi wako anaongea,” bali “sema Bwana kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”
 Sita, akaugua. Kuugua ni kupumua kwa nguvu. Alioneshwa kuguswa na matatizo ya wengine. Alimtazama kiziwi na bubu kwa huruma. Kiziwi hafokewi. Nasi hatuna budi kuguswa na matatizo yaw engine, ndipo watakuwa tayari kutusikilizwa. Saba, alisema efatha yaani funguka. Neno linaumba. Tutumie maneno kutatua matatizo ya kutosikiliza. Tutoe mwito. Tutumie matangazo na vipeperushi. Mfano palipo na soko yawekwe maneno haya. Nunu mahitaji usinunue UKIMWI. Palipo na wengi yawepo maneno haya: Ulevi noma. Mwenye masikio ya kusikia na asikie.

SURA YA SABA

MPINGA KRISTO

7.0 UTANGULIZI

Siku hizi tumekuwa katika ulimwengu wa kila kitu karibu kuwekwa ndani ya uwezo wetu. Hii yote imechangiwa na mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia. Kumbe katika kila jambo tuwe makini kabla ya utekelezaji, kwa kuchambua na kupima kipi ni kipi na kipi sicho. Na hivyo, kukubali maneno ya mtu asemaye kwamba avutwa na Roho wa Mungu sharti kuchunguza ukweli wa maneno yake.[89]

7.1 Ni halali kuamini kila Roho?

1Yoh 4:1-3 “Wapenzi, msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. Katika hili mwajua Roho wa Mungu: kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.” Kwa kutambua sasa wapinga Kristo, maana yake ni wale walio kinyume na ukweli wa Mungu; hivyo ni waongo. Mtu aliye mwongo hakika huyo hawezi kushuhudia ukweli wa Mungu, zaidi atafanya upotoshaji. “Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo. Kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. Na amri hii tumepewa na yeye: ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.” Kwahiyo, alama kwamba anampenda mtu ampenda Mungu kweli ni mapendo yake kwa jirani. Sasa kama unaweza kuwadanganya wengine ya kuwa unaponya hiki na kile, kumbe hamna mkono wa Mungu wewe ndiye mpinga Kristo.

7.2 Wapinga Kristo wapo mpaka sasa

Maana siku hizi tunaona wachungaji wakijitokeza wengi sana, na wengine kusema wamevuviwa ama wamefunuliwa na Mungu kuanzisha Kanisa fulani. Lakini utagundua ya kuwa ni wapinga Kristo pale unapowasikia wakijinadi na kutafuta wateja wale ambao hawajaimarika na kuiva kiimani kuwa waje tunaponya maradhi mbalimbali. Zaidi ya hayo katika ibada zao hutosikia neno Kristo Yesu ndani ya madhehebu au ibada zao; hao tambua ni wapinga Kristo. Ndugu yangu unayekisoma kitabu hiki, wafikishie na wengine ambao bado hawajatambua mbinu chafu wanazotumia manabii hawa wa uwongo na wapinga Kristo. Kabla ya kwenda kwao wajitahidi kuyapima na kuyachunguza maneno ya washawishi wao. Ndiyo maana zaidi utasikia wakijigamba kwa mambo yahusuyo miujiza na mengin mengi yahusuyo hayo. Wanasema itika wito kata neno, ila mimi nasema hata huo wito wa kwenda kuwasikiiza usipoteze muda wako usijeukadanganyika na kushawishiwa nao.
Lakini tutambue ya kuwa mimi na wewe tunaojiona ya kuwa tu wafuasi wake Kristo, kama maisha yetu hayafuati matakwa ya Mungu; nasi tu wapinga Kristo. Kwa mantiki hii, tunaposhindwa kufanya mapenzi ya Baba, ni sawa na kumchukua Mwana wake (yaani Yesu Kristo) na kumrudisha au kumkumbusha mateso tuliyomtendea. Japo kwake Mungu aliyatenda kwa upendo na huruma, kusudi tupate kuokolewa. Kumbe tutambue moja kwa moja, tunaposhindwa kuishi au kuyaishi yale tunayoyafahamu; tutambue kwamba tu wapinga Kristo pia. Ili sasa tuweze kujinasua na janga hilo la kumpinga Kristo, mimi na wewe tujitahidi kuishi vema na katika kweli kile tunachofundishwa Naye.  Kwani tukiendelea kumsikiliza Yeye basi anatueleza kututapotea kwani Yeye ndiye njia, kweli na uzima. Na hivyo tutabaki tumeshikamana naye mpaka huko alipotuahidia kufika, kwani tutakuwa watoto wema, waaminifu na wasiomsaliti au kumpinga Yeye aliyemtuma kwetu. Na hivyo Yesu ni njia ya kwenda kwa Baba.[90]

TUMAINI LAKO LIKO WAPI?

8.0 UTANGULIZI

Bwana asema hivi, “Amelaaniwa mtu Yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake, na moyoni mwake amemwacha Bwana. Maana atakuwa kama fukara nyikani, hataona yatakapotokea mema. Bali atakaa jangwani palipo ukame, katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.[91]
Kuna wakati kama wanadamu tunashindwa kumwona Mungu katika yale tukuanayo katika maisha. Na hii yote inachochewa na hali ya kuwategemea wanadamu wenzetu. Utasikia mara mtu fulani amekumbwa na janga, oh hapo kuna mkono wa mtu. Lakini wanashindwa kutambua ya kuwa yeye aliyeumba kila kitu ndiye mwenye mamlaka ya mambo hayo. Yesu mwenyewe anautoa mfano huo wa wagalilaya walikuwa wameuliwa na Pilato, sasa anawahadharisha ya kuwa kuuawa kwao siyo kwamba walikuwa wakosefu kupita wengine walioishi Yerusalemu. Bali ni mpango wake na hivyo mwito wake akiwata nao waliobaki watubu vinginevyo wataangamia pia. Rej Lk 13: 1-5.
Na hivyo majanga hayo tupitiayo siyo adhabu ya Mungu. Bali mambo ya kupita tu. Na hivyo tubaki kumshikilia sana Mungu kwa kuwa na matumaini kwake. Kama binadamu pale tukutanapo na matatizo basi ndiyo wasaa wa mateso, huzuni, taabu, shida, usumbufu, udhia n.k , na kujiona kuwa hatusikilizwi na watu sisi. Hapo ndipo tunakuja kuona watu wa aina mbili; Yule ambaye katika mahangaiko anamsahau Mungu naye ambaye katika mahangaikobasi ndipo anamtafuta Mungu. Kumbe tujiunge na Mwanafalsafa Simone Weil (1909-1943) Mfaransa wa mambo ya jamii aliyesema “Jinsi ilivyo vigumu kumsikiliz mtu aliye katika mateso ndivyo ilivyo vigumu kwake kutambua kuwa huruma inamsikiliza.” [92]

8.1 Yesu nakutumainia


Yesu Nakutumainia (Jesus I Trust in Yoo or Jesus I Trust in Thee), ni maneno tunayoyaona katika picha aliyoonyeshwa Mtakatifu  Sista Faustina Kowalska.

Maneno haya   yanatoa ni kwa jinsi gani maisha yetu yanapaswa kumwelekea Kristu. Kwa maneno mengine yanatupa picha halisi ya maisha yetu ya kuwa yanaaswa kumtegemea Mungu. Na hivyo daima tuanze na Mungu na kumaliza na Mungu. Kwa kufanya hivyo, hakika hatutapungukiwa na kitu. Kwani Mungu ndiye mtoa na mwezeshaji wa kila kitu. Amebarikiwa mtu Yule anayemtegemea Bwana, ambaye Bwana ni tumaini lake.[93]       


8.2 Ishara haitoshi


Kwanini tuwe watu wa kutaka tuone ishara ndiyo tuamini? Kumbuka Yesu alimwambia Thomaso ya kuwa waheri wale wasioona wakasadiki. Lakini pia tunashindwa kutambua kuwa Yesu mwenyewe alishatuambia ya kuwa hakuna ishara tena baada ya ile ya Yona.[94]  Kwa hiyo, tusing’ang’anie mambo yasiyo ya msingi.
Wakatokea Mafarisayo, wakaanza kuhojiana naye; wakitafuta kwake ishara itokayo mbinguni; wakimjaribu. Akaugua rohoni mwake, akasema, “Mbona kizazi hiki chatafuta ishara? Amin, nawaambieni: Hakitapewa ishara kizazi hiki.” Akawaacha, akapanda tena chomboni, akaenda zake hata ng’ambo.[95]
Sasa ndugu zangu ambao tumekuwa tukikimbilia na kuamini miujiza eti ya siku hizi, kweli tunamwelewa Yesu? Kuna mtu amebaki ni mtu wa kutangatanga. Ameugua tu cha kwanza cha kufikiria ni juu ya wachungaji wanaotenda miujiza. Akiamini hao watamponya. Hiyo hali binafsi naiona kama mchezo wa kuigiza tu. Kama kweli unaamini juu ya Mungu kuwa ni mweza wa yote, kwa nini usibaki ulipo na siyo mpaka kuanza kutafuta watu wa ziada? Tubadilike pia tujitambue na kuanza kujiuliza mara kadhaa. Kwa nini kuponywa kwako ni mpaka uwafuate? Mungu yuko mahali pote, na hivyo kama kweli una imani atakusaidia na kukuponya katika maradhi yako. Tusikae na kusubiri miujiza. Siyo kila kitu cha kushangaza au cha muujiza chatoka au kinatendwa na Mungu. Chunguza vizuri baadhi yao utawakuta wanatumia nguvu za giza. Sasa usipojua hayo, nawe unaenda kuwa mshirika wao. Na tambua shetani akishakukamata kujitoa ni ngumu sana. Tusikubali kuchumbiwa au kutongozwa (kushawishiwa) na shetani, ni mbinu tu anatumia kutuvutia kwake tusipokuwa imara katika imani.

8.3 Mambo ya Mbinguni yawe hamu yetu


Siku hizi mimi na wewe tumekuwa hodari sana kwa mambo ya kidunia zaidi. Kwa mfano, unamkuta kijana amekariri wimbo wa msanii fulani, anauimba mpaka unabaki  kushangaa kwamba inawezekanaje jabo hilo. Au kijana anajua kikosi cha timu fulani, kuanzia kikosi cha kwanza (First Eleven), walioko katika benchi (Subsitituion) wote. Huyo huyo kijana, anajua historia ya mchezaji fulani wa mpira au historia ya msanii fulani. Sasa cha kushangaza na cha ajabu, jaribu kumwuliza juu ya Katekesimu hakumbuki chochote. Tusiende mbali, hakumbuki wala hajui hata tarehe ya Ubatizo, Kipaimara, Komunyo ya Kwanza. Achilia hayo, mwulize juu ya Historia ya Mtakatifu Somo wake, hajui chochote. Huyu kijana ambaye anauwezo mkubwa wa kujua mambo haya mengine ya kidunia, na mbaya zaidi ni Mkristo Mkatoliki ilia mambo ya Kiroho hajui wala hakumbuki ila ya kidunia ndiyo yako mikononi mwake.
 Sasa je! Tunaenda wapi au tunalipeleka wapi Kanisa la kesho na Roho zetu tunaziandaa kwenda wapi?    Hamu yetu iwe katika mambo ya mbinguni na siyo ya kidunia. Kol 3:2

8.4 Kwanini tubaguane?


Sisi wote tu mali yake Mungu. Ubaguzi watoka wapi? Kuna wakati mwingine tunaleta mambo ya kutisha na kushangaza. Kama Wakristo kuanza uwaza na kuwekeana mipaka kwa kuangaliana; huyu kabila gani, ukoo gani, anatokea wapi, maskini, tajiri. Haya yote hayana nafasi kwa kuwa kwa Mungu wote tu sawa. Gal 3: 27-28, 1 Kor 12: 13
Kumbe hatuna sababu ya kuanza kuwekeana mipaka. Wakati kupitia kifo cha Bwana wetu Yesu Kristo basi tumekuwa na uhusiano Mwema baina yetu kwa sisi pia na Mungu. Kwa kuivunja minyororo basi amekuwa daraja kwa sisi kupita. Vivyo hivyo, nasi kama wafuasi wake tunaalikwa kuendelea kutunza na kuuishi uhusiano huu mwema. Tuishi pasipo kutazamana kijicho wal akudhaniana vibaya au kufikiriana vibaya. Tuishi kwa amani, bila kudharauliana, bila kuonyesha umaridadi, au kujiona sisi ni bora zaidi kuliko wao au wale. Tukizingatia ya kuwa wote kama Wakristu lengo letu (final destiny) ni kufikia Utakatifu mara baada ya maisha ya hapa dunaiani. Kumbe tukishindwa kuishi Upendo, hapo ndipo tunakaribisha ubaguzi na matabaka kati yetu. Ndiyo maana hata tunapoishi tutambue na kujua ya kuwa maisha siyo tu hapa duniani bali kuna maisha baada ya kifo.

HITIMISHO

Tusiwe watu wa kuitwa Nomine Christus; yaani Wakristo jina, tupambane kweli kweli. Tujifunze mfano wa Watu waliopewa  Talanta, ambapo Yesu anautoa juu ya mtu atakaye kusafiri lakini kabla ya kusafiri akawaita watumwa wake na kuweka mali zao kwao. Kuna aliyepewa Talanta tano, na mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja.  Akishakurudi akawakuta watumwa wawili wamezalisha mara mbili ya talanta walizopewa ila Yule mmoja aliyepewa talanta moja hakufanya au kuongeza chochote.[96] Kwa hiyo hao watumwa ni Wakristo. Yesu anawaachia neema zake ili wazitumie kupata matunda. Baadaye atawadai watoe hesabu ya kutumia neema zake.  Na neema hizi ndugu zangu tunazipata kupitia Sakramenti takatifu mbalimbali tuzipatazo katika kutujenga na kutuimarisha zaidi na kubakia kweli kuitwa Wakristo.
Ukristo wetu unatudai kutoa matunda. Kama Yesu alivyo mzabibu wa kweli, nasi hali kadhalika tunaalikwa kuiga kwake.[97] Mintarafu kielelezo cha mzabibu (rejea Yer 2:21; Isa 5:1) katika Injili tatu za kwanza Yesu anatumia kielelezo hicho kwa kueleza Ufalme wa mbinguni (Mt 20: 1-8, 21:28-31, 33-41). Yesu anatumia uzao wa mzabibu kwa ajili ya Ekaristi Takatifu ya Agano Jipya (Mt 26:29). Hapo Yesu anajiita mzabibu wa kweli, uzao wake utakuwa Taifa jipya teule, wala halitadanganya matumaini ya Mungu. Taifa jipya hilo litaishi katika uzima wa imani na mapendo kwa sababu wanaishi katika Kristo.  Taifa teule ndiyo mimi na wewe ambaye tunamwamini Kristo, na hivyo tu Wakristo maana tumeshikamana naye na kunamdhihirisha pale tunapofanya yale yampendezayo; na kwa kufanya hivyo Ukristo wetu utakuwa unazaa matunda.
- Gal 5: 22, 23a, 25 Matokeo ya kuongozwa na Roho ni mapendo, furaha, amani, uvumilivu……
Tufike mahali tuone matatizo ni maisha na maisha ni matatizo. Au kwa lugha nyingine tufike mahali tukubaliane na hali zetu, tusiwe watu wa kuishi maisha ya kuiga





REJEA


Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Misale ya Waamini, Toleo la Kumi, TMP Book Department, Tabora- Tanzania, 2008
Biblia ya Kikatoliki Toleo la Iringa.
Kamgisha M. Faustin, Matatizo si Tatizo, Matatizo ni Daraja, Franciscan Kolbe Press, Limuru, 2014[1]

Katekisimu ndogo ya Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Songea.
Katekisimu ya Kanisa Katoliki, Paulines Publications, Nairobi, 2000.
Mchamungu Henry, Maadhimisho ya Sakramenti kuendana na Sheria za Kanisa, Nesmap Printing Technology, Dar es Salaam, 2017.

Mtaguso Mkuu, Maelezo ya Hati 16 za Vatican II, Jimbo Kuu Tabora, Toleo la Nne 1993.
OTT Ludwig, Fundamentals of Catholic Dogma, J. C. Bastible (ed), P. Lynch (trans.), Tan books and Publishers, Inc, Rockford, 1960.
Saba Raymond, Wewe ni Kuhani Milele, Tafakari ya Mababa wa Kanisa juu ya Upadri, Toleo la Pili, Benedictine Publications Ndanda- Peramiho Tanzania, 2017.
The Code of the Canon Law, New Revisedd English Translation, Harper Collins Publishers, Newsland, 1983.


[1] Rej. MSK. 96, 204.
[2] Rej. MSK. 11.
[3] Mt 28: 18-20
[4] Ybs 27: 4-7.
[5] Ybs 8: 3.
[6] Ybs 5: 9-11.
[7] Mt 5:3-10.

[8] Ebr 7: 23-27.
[9] Rej. Mk. 9: 30-37.
[10] Ebr 5:1-5.
[11] Rej. Lk 3:23.
[12] Faustin M. Kamugisha, Matatizo si Tatizo, Matatizo ni Daraja, Franciscan Kolbe Press, Limuru, 2014, uk. 86.
[13] Rej. Yak 2:17-18.
[14] 1Yoh 1: 8-10.
[15] Mk 13: 31-33.
[16] Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Misale ya Waamini, Toleo la Kumi, TMP Book Department, Tabora- Tanzania, 2008, Uk. 920-921.

[17] Rej. Rum 8: 28-32.
[18] 1 Pet 2: 9-10.
[20] Ebr 11:1.
[21] Efe 2:8.
[22] 1Kor 2:12-16.
[23] 1Yoh 4:12-13.
[24] Ybs 2: 8-10.
[25] Mt 6:30.
[26] Mt 15:28.
[27] Lk 17:5.
[28] Mt 21:22
[29] Ebr 12:1-2
[30] Flp 4: 4,7.
[31] Rej. Rum 10:17.
[32] Rej. Rum 14:23.
[33] Rej. Mdo 5:1-11; Mith 21:27.
[34] Rum 8:28
[35] Rej. Lk 5: 1-11
[36] KKK. Na.1210.
[37] Rej. MSK Na.  845
[38] Rej. Henry Mchamungu, Maadhimisho ya Sakramenti kuendana na Sheria za Kanisa, Nesmap Printing Technology, Dar es Salaam, 2017, Uk. 1-3.
[39]Rej.  Ibid. Uk. 8-10.
[40] Muhtasari, KKK. Na. 1133.
[41] Rej. Mt. Toma wa Akwino, Summa Theologica III, 65, 3.
[42] Rej.  MSK. Na.1055.
[43] Rej. MSK. Na. 1056.
[44] Katekisimu ndogo ya Kanisa Katoliki, Uk. 48.
[45] Rej. KKK Na.1213
[46] Rej. KKK. Na.1212
[47] Rej. Mt 28:19.
[48] Ibid.
[49] Rej. KKK. Na. 850.

[50] KKK. Na. 1315.

[51]KKK. Na.1250.
[52] Rej. Mdo 16:15, 33, 18: 8; 1Kor 1:16.
[53]Rej. 1Tim 2: 4, Mk 10:14.
[54] Rej. KKK. 1246, MSK. Na. 864.
[55] Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Misale ya Waamini, Toleo la Kumi, TMP Book Department, Tabora- Tanzania, 2008, Uk. 910.

[56] Rej. Rum 6: 3-11; Kol 3: 1-4.
[57] KKK. Na. 1316.

[58] Ibid, Na. 1319

[59] Ibid, Na 1320

[60] Ibid, Na  1321

[61] Rej. MSK. Na. 879.
[62] Rej. MSK. Na. 880 § 1.
[63] REJ. Ibid. § 2.
[64] Rej. MSK. 886 § 1.
[65] Rej. Ibid. § 2.
[66] Rej. MSK. Na. 881.
[67] Rej. MSK. Na. 884 § 2.

[68] Ibid, Na 1313

[69] Rej. MSK. Na. 88.
[70] Yn 6: 51, 54, 56.
[71] Mt 26: 26-28, Mk 14: 22-25; Lk 22: 19-20, 1Kor 11: 17-32.
[72] Rej. Yn 6:1-68.
[73] Mdo. 2:42; 20:7.
[74] Apolojia ya kwanza 66.
[75] DS. 1740.
[76] Rej. Henry Mchamungu, Maadhimisho ya Sakramenti kuendana na Sheria za Kanisa, Nesmap Printing Technology, Dar es Salaam, 2017, Uk. 58, 85.
[77] KAOMBE STEFANO,Misa Takatifu, Adhimisho na Maisha , Epiklesis, uk. 93
[78] Rej. Ybs 32:19.
[79] Rej. MSK. Na. 1091.
[80] Rej. Yoh 20:21-23.
[81] Rej.  KKK. Na. 1499.
[82] Hes 11:25. 
[83] Hes 15:17.
[84] Rej. Hes 27:18 -23.
[85] Rej. Amu 3: 7-11.
[86] 1 Yoh 2:12-16
[87] 1 Yoh 4:5.
[88] Rej. Mk 7:33.
[89] Rej. 1Kor 12:10.
[90] Rej. Yn 114: 1-6.
[91] Yer. 17:5-6.
[92] Rej. Faustin M. Kamgisha, Matatizo si Tatizo, Matatizo ni Daraja, Franciscan Kolbe Press, Limuru, 2014, Uk. 47.
[93] Yer. 17:7
[94] Rej. Mt 12: 38-39.
[95] Mk 8: 11-13.
[96] Rej. Mt 25: 14-30.
[97] Rej. Yn 15: 1-11.