TUCHUNGULIE UBONGONI MWA MWANADAMU BILA UPASUAJI,
KAZI NZURI NI IPI DUNIANI?
MBAGALA SPIRITUAL CENTER ,DAR
@ LIBERIO S.BAVUGUBUSA C.
KAZI NZURI NI IPI DUNIANI?
MBAGALA SPIRITUAL CENTER ,DAR
@ LIBERIO S.BAVUGUBUSA C.
Swali huenda likatuchanganya kabisa,au tuseme kuna kazi mbaya? Muuliza swali huenda angeuliza kazi harali na kazi isiyoharali.
Hata hivyo ,Ni vema kuwa mwaminifu kwa muuliza swali.Nakumbuka nikiwa shule ya msingi Mabamba ,Kibondo wilayani wakati huo shule ikiitwa Misheni.
Tulikuwa tukisoma kwa mashindano ili kila mmoja awe wa kwanza darasani.Nilifuata maelekezo ya Baba yangu alivyoniambia " Kamwe Shuleni mwanangu usiwe rafiki wa mambulula" watakubwetesha. Na hapo nikajichagulia marafiki wasio "mbulula"(wenye uwezomdogo darasani).
Kati ya wanafunzi darasa la Pili na la nne waliojiweza walikuwa kama wafuatao, Valeriani Mbweja, Verasius W.Teyumwete, Julius Batromeo( mtoto wa mkulima), Victor na Dickson A. Kibala, Adili Husein Tamim, Simon Njuguma,Tausi Athuman,nk. Hao walikuwa ni vikolezo vya kuhamasishana kufanya vizuri darasani.
Mara kadhaa tulijikumbusha ule wimbo wa akina Baraka,Neema na Misa, " What are you going to be " ? Maana yake Unataka kuwa Nani? Mmoja alijibu angependa kuwa "Mwalimu", mwingine alijibu angependa kuwa "nesi" ,Mwingine alipenda kuwa "mkulima".Kwa akili zanguza kitoto niliamini kuwa kila mmoja alichagua kazi aliyoipenda zaidi kuliko ile ambayo hakuitaja.
Hiyo ni mifano hai mara nyingi ninaitumia katika kuinuana kifikra, kiuchumi na kiutendaji.
Marthin Luther Jr. Mmarekani mweusi na Mwanaharakati wa haki za watu weusina wenye asili ya Afrika na walatino aliwahi kutushauri katika maisha kwa ujumla kuwa katika maisha kuna Mambo yatakayokufanya ufike pale ambapo ungependa kufika.
Moja,Ufanye kazi unayoipenda.Kimsingi Anza na kile unachopenda japo si mbaya ukafanya kile unachopendekezewa hasa "wahenga" wakubwa wako wameonelea kipaji ndani mwako.Ninampenda sana Mheshimiwa huyu na Mwanaharakati huyu Marthin Luther Jr,mawazo yake katika pointi hii amefanana na Mzee Gotama Budha aliyewahi kusema "Tunakuwa hivi kwa KUTOKANA na mawazo yetu" ndio kusema tuko hivyo kutokana na mawazo yetu. Ambapo Mwanafasafa wa Kichina Confucius katika karne ya 5 kabla ya Kristo anasema " Ukitaka kufanya Jambo lifanye kwa moyo, na ulitaka kwenda mahali nenda kwa moyo". Kumbe hata wahenga waliliona kwa kusisitizia kuwa hatunabudi kuchagua chaguo letu wenyewe. Ukifanya kazi ya kuchaguliwa binafsi naifananisha na la kuchaguliwa mchumba ili awe mama yoyo. Kumbe ni vema kufanya kile unachokipenda.Hiyo kazi unayoipenda ndio kazi yako nzuri.Kama sio nzuri ieache ili ukalime lami.Kishapo ujipimie mwenyewe joto la jiwe.Ndipo akili zitakapokusogea na kugundua ukweli wa Falsafa ya kutafuta kazi nako ni kazi.
Hata hivyo ,Ni vema kuwa mwaminifu kwa muuliza swali.Nakumbuka nikiwa shule ya msingi Mabamba ,Kibondo wilayani wakati huo shule ikiitwa Misheni.
Tulikuwa tukisoma kwa mashindano ili kila mmoja awe wa kwanza darasani.Nilifuata maelekezo ya Baba yangu alivyoniambia " Kamwe Shuleni mwanangu usiwe rafiki wa mambulula" watakubwetesha. Na hapo nikajichagulia marafiki wasio "mbulula"(wenye uwezomdogo darasani).
Kati ya wanafunzi darasa la Pili na la nne waliojiweza walikuwa kama wafuatao, Valeriani Mbweja, Verasius W.Teyumwete, Julius Batromeo( mtoto wa mkulima), Victor na Dickson A. Kibala, Adili Husein Tamim, Simon Njuguma,Tausi Athuman,nk. Hao walikuwa ni vikolezo vya kuhamasishana kufanya vizuri darasani.
Mara kadhaa tulijikumbusha ule wimbo wa akina Baraka,Neema na Misa, " What are you going to be " ? Maana yake Unataka kuwa Nani? Mmoja alijibu angependa kuwa "Mwalimu", mwingine alijibu angependa kuwa "nesi" ,Mwingine alipenda kuwa "mkulima".Kwa akili zanguza kitoto niliamini kuwa kila mmoja alichagua kazi aliyoipenda zaidi kuliko ile ambayo hakuitaja.
Hiyo ni mifano hai mara nyingi ninaitumia katika kuinuana kifikra, kiuchumi na kiutendaji.
Marthin Luther Jr. Mmarekani mweusi na Mwanaharakati wa haki za watu weusina wenye asili ya Afrika na walatino aliwahi kutushauri katika maisha kwa ujumla kuwa katika maisha kuna Mambo yatakayokufanya ufike pale ambapo ungependa kufika.
Moja,Ufanye kazi unayoipenda.Kimsingi Anza na kile unachopenda japo si mbaya ukafanya kile unachopendekezewa hasa "wahenga" wakubwa wako wameonelea kipaji ndani mwako.Ninampenda sana Mheshimiwa huyu na Mwanaharakati huyu Marthin Luther Jr,mawazo yake katika pointi hii amefanana na Mzee Gotama Budha aliyewahi kusema "Tunakuwa hivi kwa KUTOKANA na mawazo yetu" ndio kusema tuko hivyo kutokana na mawazo yetu. Ambapo Mwanafasafa wa Kichina Confucius katika karne ya 5 kabla ya Kristo anasema " Ukitaka kufanya Jambo lifanye kwa moyo, na ulitaka kwenda mahali nenda kwa moyo". Kumbe hata wahenga waliliona kwa kusisitizia kuwa hatunabudi kuchagua chaguo letu wenyewe. Ukifanya kazi ya kuchaguliwa binafsi naifananisha na la kuchaguliwa mchumba ili awe mama yoyo. Kumbe ni vema kufanya kile unachokipenda.Hiyo kazi unayoipenda ndio kazi yako nzuri.Kama sio nzuri ieache ili ukalime lami.Kishapo ujipimie mwenyewe joto la jiwe.Ndipo akili zitakapokusogea na kugundua ukweli wa Falsafa ya kutafuta kazi nako ni kazi.
Kazi nzuri ni ipi, ni ile ambayo itakudai Ufanye kwa bidii tena kwa masaa kibao.Kama Wachina hufanya kazi masaa mengi,mpaka kituo cha haki za kibinadamu Amnesty huthubutu kuingilia Kati kwani wao hufanya kazi kwa Falsafa ya "punda afe mzigo ufike" ningewatania akina " hung yang ping" kwamba hufanyakazi Kama watumwa wakilenga kumkimbiza "kidume" cha Dunia ndio Waamerika ambao juzi Rais Donald Trump alijinasibu kwa ngembe nyingi kuwa katika utawala wake ameirudishia heshima tena Amerika.Ha ha ha kibwagizo cha wiki hiki.
Mwanaharakati Marthin Luther anasema, kazi uipendayo ifanye kwa muda wa kutosha na zaidi ya yote kwa ueledi mkuu.
Kazi nzuri ni ile utakayotaka kuifanya ili mwisho wa siku "utusue" utoboe ,ama uyaone matunda yake Tena waziwazi kwa kuacha Falsafa au "legacy" kwa kimombo. Usifanye kazi ilimradi utokwe na jasho, jasho haliuzwi hata ukipiga "push up" au ukala pilipili za wahindi jasho litakutoka. Kazi nzuri itakudai kuhenyeka kweli.Itakutaka uifanye kwa moyo.
Mwanaharakati Marthin Luther anasema, kazi uipendayo ifanye kwa muda wa kutosha na zaidi ya yote kwa ueledi mkuu.
Kazi nzuri ni ile utakayotaka kuifanya ili mwisho wa siku "utusue" utoboe ,ama uyaone matunda yake Tena waziwazi kwa kuacha Falsafa au "legacy" kwa kimombo. Usifanye kazi ilimradi utokwe na jasho, jasho haliuzwi hata ukipiga "push up" au ukala pilipili za wahindi jasho litakutoka. Kazi nzuri itakudai kuhenyeka kweli.Itakutaka uifanye kwa moyo.
Kazi nzuri ni ile utakayokuwa umejiwekea malengo ya kukukombowa.Katika Kitabu kilichoandikwa na Robert T. Kiyosaki, "Rich Dad and Poor Dad'' kinaonesha tofauti ya mtazamo wa Mtoto wa mkulima(poor Dad) tuseme yeye anakwenda Shuleni ili aajiliwe huku mtoto wa Rich Dad (Tajiri) anakwenda shule ili ailinde pesa kiusomi na sio apate kazi ya kuajiliwa na mtu.Anakwenda shule ili apate akili zaidi ya kuilinda pesa asifilisike mpaka kizazi cha nne ndio hao wafanyabiashara Waasia. Wabongo sehemu kubwa tunajua kutafuna pesa tulizoachiwa KWENYE mirathi na uzuri wa Bahati pesa za mirathi tunazitafuna bila kuzihurumia,kwa kigezo kilekile cha kuzipata kwa nasibu na bila kuzihangaikia.Ndio kisa pesa za mirathi hazilipi na hazikufanyi uumize kichwa.
Lao Tse Tzu MDAU mkubwa wa Falsafa za akina Confucius aliwahi kusema katika kazi nyepesi jiandae kukutana na magumu ili uifanye kwa ueledi mkubwa na umakini. Huyu Mwanafasafa Mchina anataka kutukumbusha tufanye Mambo kwa umakini yaani "serious". Maandiko matakatifu yametoa "ole" kwa wale wajiaminio kipumbavu. Ole wao wajiaminio kipumbavu, Upumbavu ni uparambogo,kutaka kujifanya unajua huku hujui na hutaku kujua wala kufundishwa.
Maisha na kazi ningesema ni sawa na kuwa na barabara nzuri zimetengenezwa kwa ajili ya magari huku hakuna magaru na watu wenyewe waamue kupita vichakani. Wajerumani walikuwana Falsafa ya kupiga kazi na sio kubwabwaja midomo.Ndio kusema Matakatifu Benedikto alisisitiza juu ya Sala na kazi na sio kulialia bila kupigwa.Tuchape kazi bwana.
Turudi sasa kwenye simulizi la vijana Musa, Baraka na Neema.
Yule aliyesema, ATAKUWA MWALIMU.
Huyu atapaswa kurithisha Elimu toka kizazi hata kizazi.
Huyu atahitaji awe mwema na atapasika kuwa Mfano Bora kwa watoto na jamii.
Atapaswa akwepe madeni yasiyo na tija.
Atapaswa kujiwekea uzeeni hasa kwa kutunza pensheni zake.
Atapaswa kuwakwepa walevi wa mjini na vijijini.Kwani pensheni ikiisha wao ndio watakaokuwa wakwanza kukupiga majungu na kukuona mpuuzi wa mwaka.
Atapaswa ajenge nyumba ndani ya miaka kumi ya kwanza ya kuajiliwa.
Atapaswa awekeze pesa benki ikiwa ni Maandalizi ya Kuandaa ada za watotoAtapaswa anunue mashamba walau Kama ni ekari chache ziwe kumi na tano au zaidi.Panda miti itakyokoa uzeeni. Ningekuwa Mwalimu ningefanyaje? Historia inaonesha kuwa walimu husahaulika msinite Mwanaharakati " sitaki" wengi hata walionifundisha nawaona walivyo na maisha duni.Mitazamo duni.Makazi duni.Chakula duni.Mshahara kuisha katikati ya mwezi.
Nifanyeje.Kukuruka.Fuga kuku vijana wa kazi watabaki wanawatazama kwani ukichelewa kazini ' majipu" yatashughulikiwa. Pensheni ni ya kula kidogokidogo na sio gawio la ukoo.
Wote wawili waliotaka kuwa nesi na mkulima kiufupi nesi akidhi maadili ya utabibu, mkulima naye apambane na Kilimo cha tija, kulima kwa wakati, kupanda MBEGU Bora na tena kupanda mbegu katika mvua za mwanzo kama Hayati Mwl.Julius K.Nyerere alivyowashauri watanzania.
Maisha na kazi ningesema ni sawa na kuwa na barabara nzuri zimetengenezwa kwa ajili ya magari huku hakuna magaru na watu wenyewe waamue kupita vichakani. Wajerumani walikuwana Falsafa ya kupiga kazi na sio kubwabwaja midomo.Ndio kusema Matakatifu Benedikto alisisitiza juu ya Sala na kazi na sio kulialia bila kupigwa.Tuchape kazi bwana.
Turudi sasa kwenye simulizi la vijana Musa, Baraka na Neema.
Yule aliyesema, ATAKUWA MWALIMU.
Huyu atapaswa kurithisha Elimu toka kizazi hata kizazi.
Huyu atahitaji awe mwema na atapasika kuwa Mfano Bora kwa watoto na jamii.
Atapaswa akwepe madeni yasiyo na tija.
Atapaswa kujiwekea uzeeni hasa kwa kutunza pensheni zake.
Atapaswa kuwakwepa walevi wa mjini na vijijini.Kwani pensheni ikiisha wao ndio watakaokuwa wakwanza kukupiga majungu na kukuona mpuuzi wa mwaka.
Atapaswa ajenge nyumba ndani ya miaka kumi ya kwanza ya kuajiliwa.
Atapaswa awekeze pesa benki ikiwa ni Maandalizi ya Kuandaa ada za watotoAtapaswa anunue mashamba walau Kama ni ekari chache ziwe kumi na tano au zaidi.Panda miti itakyokoa uzeeni. Ningekuwa Mwalimu ningefanyaje? Historia inaonesha kuwa walimu husahaulika msinite Mwanaharakati " sitaki" wengi hata walionifundisha nawaona walivyo na maisha duni.Mitazamo duni.Makazi duni.Chakula duni.Mshahara kuisha katikati ya mwezi.
Nifanyeje.Kukuruka.Fuga kuku vijana wa kazi watabaki wanawatazama kwani ukichelewa kazini ' majipu" yatashughulikiwa. Pensheni ni ya kula kidogokidogo na sio gawio la ukoo.
Wote wawili waliotaka kuwa nesi na mkulima kiufupi nesi akidhi maadili ya utabibu, mkulima naye apambane na Kilimo cha tija, kulima kwa wakati, kupanda MBEGU Bora na tena kupanda mbegu katika mvua za mwanzo kama Hayati Mwl.Julius K.Nyerere alivyowashauri watanzania.
No comments:
Post a Comment