Thursday, February 6, 2020

MADINI YA NDOA

MADINI KUTOKA FHWF
______________________________________________

TOFAUTI KATI YA VIVUTIO VYA NDOA NA VIGEZO VYA NDOA

Tarehe: 06/02/2020, Alhamisi.

Mtunzi: Mr. Francisco Kagoma, Founder na CEO wa FHWF, Mwanafalsafa, Mwanasaikolojia, na Mshauri wa Changamoto Mbalimbali za maisha zikiwemo na ndoa.

👉🏽👉🏽👉🏽 Washirikishe wengine nao wapate MADINI motomoto kutoka FHWF, tuma maneno "MADINI YA NDOA NA FAMILIA" kwa Ma-Admin wa FHWF: Chief Admin +255767 818 542 na Co-Admin +255 716 669 895 ili wakuunganishe na FHWF (JUKWAA). SHEA SASA HIVI⤴️↗️

Habarini za leo wanandoa waliomo katika Ndoa tayari na wanandoa watarajiwa.

Wapo tunaochanganya kati ya vivutio vya ndoa na vigezo vya ndoa kama vile vingekuwa kitu kimoja. Ni ukweli kwamba vyote vina mchango wake katika ndoa.

Utasikia maneno kama una vigezo vya kuwa MKE au mume wangu? Na mtu haulizi eti una vivutio vya kuwa MUME au mke wangu? Tayari hapo kuna maana fulani inaingia ambayo inavitofautisha "vigezo" na "vivutio."

Licha ya kwamba "vigezo" huonekana kuwa na uzito zaidi kuliko "vivutio", dunia hii ingekuwa inayokera sana kwa maana tumeumbwa kwa namna inayovutia halafu eti nje yetu kusiwepo vivutio.🤷🏼‍♂️🤷🏼‍♀️

Kifalsafa, hapa tunaongea kuhusu substance (kiini/ kigezo) (what makes something/ somebeing to be what it is, yaani _kile kinachokifanya kiwe kilivyo_) na accident (kivutio) (what adds value or falls marginally to the thing, yaani kile kinachoboresha au kinachoongeza uthamani wa kitu). Inawezekana kiini na kigezo visiwe na maana sawa mathalani maana ya ndoa - kiini cha ndoa, au vigezo vya ndoa- maana hata katika matumizi hutumika vigezo vya ndoa au vigezo vya kuoana na sio kiini cha ndoa au kiini cha kuoana. Vigezo vya ndoa hukupeleka moja kwa moja kwenye dhana ya ndoa yaani kwenye kiini cha ndoa.

Tumewahi fundisha kupitia makala mbalimbali kuhusu ndoa ni nini mfano makala ya tar. 10/02/2019 NDOA NI NINI?. Tulisema hivi ndoa ni agano kati ya mwanaume (a man) na mwanamke (a woman) kuwa wanafungamana na kuungana ili kuwa mwili MMOJA, moyo (hisia) MMOJA, akili MOJA na roho MOJA, kwa ujumla kuwa kitu kimoja katika nyanja zote na nyakati zote za maisha yao au uhai wao. Tulikwisha toa ufafanuzi wa maana hiyo katika nyakati tofauti tofauti, usitoke jukwaani tovuti (fuhuwi.com) ikikamilika utaweza rejea tena.

Leo tuone tofauti iliyopo kati ya vivutio vya ndoa na vigezo vya ndoa

1. Tofauti katika dhana au maana

Dhana ya kivutio (attractive/ exciting thing) husema kivutio ni kile kinachotakiwa kuwepo au kilichopo tayari ili kukuhamasisha kufanya kitu fulani/ kufikia jambo fulani. Na dhana ya kigezo (criterion/ requirement) husema kigezo ni kile kinachotakiwa kuwepo ili jambo fulani lifanyike au lipatikane kwa usahihi.

Hivyo vivutio vya ndoa ni yale yanayayotakiwa kuwepo  au yaliyopo tayari ili kukuhamasisha kuitafuta ndoa na kuipata yaani kumtafuta na kumpata mwenzi wa ndoa, kumtafuta na kumpata mvulana au msichana fulani na kufunga naye ndoa.  na vigezo vya ndoa ni yale yanayotakiwa kuwepo ili kuwezesha ndoa ipatikane, ifungwe na idumu.🌝

2. Tofauti katika ulazima na umuhimu.

Vivutio vya ndoa si lazima viwepo bali ni muhimu kwani ndio vichocheo kwa vijana kuingia ndani ya ndoa, huiongezea ndoa thamani na kuipa ndoa hii radha tofauti na nyingine. Ndoa ni moja ila inavyojidhihirisha kwa wanandoa hawa ni tofauti na kwa wanandoa wengine. Vivutio vya ndoa huifanya ndoa iwe na sura au taswira nyingi za kuitazama au kujidhihirisha kwa watu.

Vigezo vya ndoa ni ni vya lazima kwani vikifuatwa ipasavyo ndivyo vinavyowasaidia wanandoa kukifikia kiini cha ndoa kilichoelezwa kwenye maana halisi ya ndoa (unini wa ndoa) - muunganiko kimwili, kihisia (kimoyo), kiakili na kiroho.

3. Tofauti katika kutumikiana

Vivutio vya ndoa na vigezo vya ndoa vyote hutumikia ndoa, vina mchango wake katika kuhakikisha ndoa zinaanzishwa, zinakuzwa, zinakomaa, na kuzaa ndoa nyingine (kuzaa wanandoa wengine).

Lakini vivutio vya ndoa hutumika zaidi katika kuanzisha wazo la ndoa kwa vijana, na kulichochea. Huwezesha kuanza kutafakari vigezo vya ndoa, vya kuoana ni vipi. Hivyo huwezesha vigezo vya ndoa kutafutwa na hata kumpeleka kijana katika kiini cha ndoa.

👉🏽 Vivutio vya ndoa ➡️ Vigezo vya ndoa ➡️ Kiini cha ndoa

Vivutio vya ndoa hutumikia kiini cha ndoa kupitia vigezo vya ndoa LAKINI vigezo vya ndoa hutumikia kiini cha ndoa moja kwa moja.

Nahitimisha makala hii kwa kusema kuwa vigezo vya ndoa hubaki ndani ya kiini cha ndoa, kiini cha ndoa na  vigezo vya ndoa ni kama pete na kidole, ila *vivutio vya ndoa* hubaki nje ya ndoa, huipamba ndoa, huipa ndoa  muonekano unaovutia.

Tuvipambanue vizuri vigezo vya ndoa na vivutio vya ndoa ni vipi ili tupate kutengeneza ndoa bora.

Makala zijazo zitavipambanua vigezo hivyo na vivutio hivyo ni vipi. Baki JUKWAANI _yajayo ndani ya FHWF na FUHUWI (fuhuwi.com) yanafurahisha na kuelemisha._

© Future Husbands &Wives Forum (FHWF), 2019 - 2020

No comments: