SAIKOLOJIA YA MAISHA Na.Fr.SIMON R.LIBERIO, MWALIMU WA SAIKOLOJIA
MAISHA YA MWANADAMU YANAMUHITAJI MWANADAMU MWENZAKE
Saikolojia ya maisha ya mwanadamu ina Mambo mengi.Katika maisha ya mwanadamu Kuna Mambo mengi yanayokutuletea furaha au msongo kwa jina maarufu "stress". Kuna mengi sana duniani yenye kufurahisha.Kuna mengi duniani yanaweza kukukatisha tamaa.Kuna mengi duniani yanaweza kupunguza kasi na munkali wa kuleta Maendeleo tungeita KISAIKOLOJIA " kususia" au kususa. Mwanadamu ameumbwa kichwani mwake kumejaa kama stoo ya maboksi mbalimbali.
Maisha ya mwanadamu Duniani yanaweza kuwa mafupi au marefu.Mwanadamu wa Zama zetu za utandawazi, utandawizi, na utandawazimu.
MAMBO YANAYOWEZA KUKUPATIA UTULIVU WA MOYO KATIKA MAISHA.
1.FANYA UNACHOKIPENDA MAISHANI
Maishani kuna mambo mengi na vivutio hi vingi.Wataalamu husema, " Mirusi mingi humpoteza mbwa". Ukiishi bila malengo siku zote utabaki mtu wa kushika Hiki unaacha kila kitu.
2.Maishani jitahidi kufanya kazi kwa bidii na ujipatie riziki ya kila siku.Uache kuwa mtu wa kulaumulaumu.Acha kulaumu laumu watu.
3.MAISHANI ISHI MAISHA YAKO /ZAKUAMBIWA CHANGANYA NA ZA KWAKO (J.K)
Uishi maisha yako mwenyewe.Badala ya kumlaumu aliyekunyima chakula. Tafuta mbinu halari za kupata chakula chako.Azima hata madum chota maji.Uza maji hautalala njaa.Omba vibarua hata vya kulima mashambani hautalala njaa. Ukishangaa mjini utalima lami. Dunia ni gunia hakuna atakayekuhurumia kwa uvivu na kupuuza fursa. Hata Mimi sitakuonea Huruma kwa Upumbavu wako wa kufikiri kuwa maisha ni "isidingo" au "ze comedy".
4.UWE MBUNIFU KATIKA UJASIRIAMALI
Ulimwengu huu sio wa Bibi yako. Ni ulimwengu wa watu tena wwshindani.Ujasiriamali mwingi. Biashara kwa wingi. Siasa uchwara nyingi. "Figisufigisu" nyingi. roho mbaya nyingi. roho za mtakafujo.roho za mtaka vyote. roho Mtakavitu.Ndiye anayeutawala ulimwengu wa nope nikupe. roho msakatonge.roho gombania madaraka. roho gombania vyeo. roho mchafu wivu.Dunia ina mtima nyongo. Marekani haiwezi ikacheka cheka na Taifa la uchina na kinyume chake ni sahihi. Urusi haiwezi ikachekacheka na Taifa la Amerika na kinyume chake ni sahihi.Ndio hapo tunaweza tukakibaliana kuwa adui wa bodaboda ni bodaboda. Adui au hasimu wa mfanyakazi ofisini ni mwenzake hasa wafanyakazi wavivu, wakosa ubunifu.Waiba vyeti vya mitihani.Waingia kazini kupitia migongo ya baba na wajomba zao.Watu wanamna hii usiwape taarifa za Maendeleo yako.
5.MAHATMA GHANDI ALISEMA " KAMA HAUNA SURA YA KUTABASAMU KAMWE USIANZISHE DUKA ".
Saikolojia ya muuzaji na mnunuzi ni mguso na ukaribu wa watu wawili.Mwwnye kuhitaji huduma na mwenye hitaji wa "shekeri". Mfanyabiashara anapaswa kuwa mnyenyekevu. Angalieni wachaga hapa Tanzania. Mteja si mfalme tu bali Ni ndugu alisema Baba yangu Mzee Liberio Bahanza hotelini nyumbani Mabamba.
6. TAMBUA VIPAJI VYAKO KISHA KIFANYIE KAZI KIPAJI UNACHOKIONA KINATOA MATUNDA WAZI
Kama mwanzo nilivyoandika kuwa " kichwa cha mwanadamu kimesheheni maboksi mengi yenye fikra pembuzi nyingi". Kichwa cha mwanadamu na moyo wake hujazwa na ndoto kibao. Ndoto nyingi bila kuzitekeleza ni sawa na kuwa na meno yote tena mabovu.
7. SHIKA JAMBO MOJA NA ULISHIKILIE,KIFANYIE KAZI, PAMBANA, LIWEKEA VIPAUMBELE
Maisha yanadai utulivu. Ishi kwa kutimiza ndoto zako. Ifanyie kazi ndoto yako moja ya kwanza kishapo jiulize je ninachokifanya kinanipatia raha na utulivu wa moyo? Ili kuamini kile unachokifanya kinakupatia amani ni pale unaporidhika hapo ulipo hata kama si kwa kipato kikubwa sana, angalau unaweza ukajipatia mahitaji ya msingi yaani :Makazi nadhifu, chakula bora, maji safi, mavazi, ada ya kulipa kwa watoto shuleni kwa wenye watoto au unaoweza kuwasaidia.
8. JITAHIDI KUWAVUMILIA WATU WENYE "TABIA NGUMU" (HARD CHARACTER PEOPLE) AU "SPECIAL CHARACTER PEOPLE /COMPLICATED BEHAVIOUR.
Ninapoandika kuwavumilia watu wasumbufu na wenye tabia ngum. Yapo makundi mengi ya watu wenye tabia zao ngumu. Wapo walalamishi kwa kila Jambo.Wapo wanaopinga kila Jambo.Watu wa namna hii wanashida kichwani. Au uelewa wao wa kifikra ni mdogo sana. Watu wanamna hii hawana mpanuko mkubwa wa kimawaz. BeNa be hawana "exposure" tuseme ni washamba wa Mambo mengi. Hujifanya wajuaji wa kila jambo. Wapo wanaopenda wawajali huku wao hawana muda na wenzao. Wanaopenda kubembelezwa huku wao hawana muda na mtu. Wapo wanaopenda kuhurumiwa huku wao hawako tayari kuhurumiwa. Wapo wanaopenda waheshimiwe huku hawawaheshimu wenzao. Wapo wanaolalamikia wenzao huku wao ni mizigo kwa watu.Wapo wanaotaka kusikilizwa huku hawako tayari kuwasikiliza wenzao.
9.TIMIZA NDOTO ZAKO HAKUNA MWINGINE "WEWE"
Furaha yako itapambwa pale utakapokuwa umeishi ndoto zako, ni Kama katika Maandiko Matakatifu Mzee Simeon anatoa shukrani kwa Mungu kwakumvumilia akaishi maisha marefu sana mpaka amwone Masiha wa Bwana.Anasema "Sasa Bwana WAWEZA kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani kwakuwa macho yangu yameuona wokovu wa Mungu wetu.
10. Epuka kujitengenezea maadui wako mwenyewe.Uwe na kauli njema. Uwe na simile. Mtu mzima hspigwi viboko. Mtu mzima huambiwa kiutu uzima.Hakaripiwi Kama dogo wa darasa la kwanza
11.Uwe tayari KUYAPOKEA Mambo magumu.Na zaidi ya yote ubaki na hekima ya Dini na Falsafa ya Watao kutambua kuwa unaweza ukavae koti au Sweta lakini hauwezi kuiondoa baridi. WAWEZA kuwasha taa na umeme lakini hauwezi kuiondoa Giza. Mwisho,Pokea hekima.@Fr.SIMON R.LIBERIO
No comments:
Post a Comment